Erdogan

Rais Recep Tayyip Erdoğan alielezea wasiwasi wake juu ya kuongezeka kwa mashambulizi katika ukingo wa magharibi unaokaliwa kwa mabavu akisisitiza umuhimu wa kuzuia uchochezi katika msikiti wa al-Aqsa.

Rais Erdogan wa Uturuki na Rais wa Israel Isaac Herzog walijadili uhusiano wa nchi hizo mbili katika mazungumzo ya simu mwishoni mwa Jumatatu, kulingana na kitengo cha mawasiliano.

Kwa mujibu wa taarifa ya kurugenzi ya mawasiliano ya Uturuki siku ya Jumanne, Herzog alimpongeza Erdogan kwa mwezi mtukufu wa Kiislamu wa Ramadhani, huku rais wa Uturuki akimpongeza mwenzake wa Israel kwa sikukuu ya Pasaka ya Kiyahudi.

Akiishukuru Israel kwa mshikamano na uungaji mkono wake baada ya tetemeko kubwa la ardhi mwezi uliopita kusini mwa Türkiye, Erdogan pia alisisitiza azma ya Ankara ya kuimarisha uhusiano.

Erdogan alizidi kuwasilisha "wasiwasi wake" juu ya kuongezeka kwa mashambulizi na vitendo vya unyanyasaji katika ukingo wa Magharibi wakati Ramadhani inakaribia, kulingana na taarifa.

Alisisitiza umuhimu wa kutoruhusu uchokozi na vitisho dhidi ya hadhi ya kihistoria na hali ya kiroho ya msikiti wa al-Aqsa katika Jerusalem Mashariki inayokaliwa kwa mabavu.

Taarifa hiyo pia ilibainisha kuwa Erdogan alimshukuru Herzog kwa jitihada zake za kuhifadhi utulivu na hali ilivyo.

TRT Afrika