Washiriki wa madhehebu ya Kenya wapatikana wamekufa baada ya 'kufunga kwa ajili ya Yesu' / Picha: AFP

Wataalamu wa uchunguzi nchini Kenya wameanza zoezi la uchunguzi wa maiti zaidi ya mia moja zilizopatikana kwenye makaburi ya halaiki zilizohusishwa na mchungaji anayedaiwa kuwaagiza wafuasi wake kufa kwa njaa.

"Rasmi shughuli ya uchunguzi wa miili inaanza mara moja," Waziri wa Mambo ya Ndani Kithure Kindiki aliwaambia waandishi wa habari nje ya chumba cha kuhifadhia maiti cha hospitali katika mji wa pwani wa Malindi siku ya Jumatatu.

"Tuko hapa kushuhudia hatua muhimu sana," alisema. "Mchakato huo unatarajiwa kuchukua takriban wiki, yote yanakwenda vizuri."

Wachunguzi pia watachukua sampuli za DNA kusaidia utambuzi, ingawa matokeo kamili yanaweza kuchukua miezi, daktari mkuu wa serikali, Johansen Oduor, alisema.

Makaburi ya watu wengi katika msitu ulio karibu wa Shakahola yamefichua watu wengi waliofariki, wengi wao wakiwa watoto, shirika la habari la AFP linaripoti.

Lakini baadhi ya wale 109 walioripitiwa kufa, ambayo inajumuisha idadi ndogo ya watu ambao walipatikana wakiwa hai lakini walikufa wakiwa njiani kupelekwa hospitalini, idadi yao inaweza badilika.

“Mchakato wa ufukuaji ulisitishwa kwa muda kwa sababu wataalamu walitushauri (kwamba) wakati wa mvua, mchakato huo hauwezi kuendelea,” Kindiki alisema.

Paul Mackenzie Nthenge, dereva wa zamani wa teksi ambaye alianzisha dhehebu la Kikristo liitwalo Good News International Church, anashutumiwa kwa kuwaambia wafuasi kwamba njaa inayoosha njia kuelekea kwa Mungu.

Lakini Kindiki alisema Ijumaa kuwa ripoti za awali zilidokeza "kwamba baadhi ya wahathiriwa huenda hawakufa kwa njaa. Kulikuwa na mbinu nyingine zilizotumika, ikiwa ni pamoja na kuwaumiza."

Kugunduliwa kwa miili hiyo kulishtua sana Kenya -- athari iliyoongezwa wiki iliyopita na tangazo kwamba mwinjilisti mwingine mashuhuri atashtakiwa kwa "mauaji ya watu wengi" ya wafuasi wake.

Ezekiel Odero, mkuu wa New Life Prayer Centre and Church, ambaye alikamatwa siku ya Alhamisi, anashukiwa kwa uhalifu ikiwa ni pamoja na mauaji, kusaidia watu kujiua, utekaji nyara, itikadi kali, uhalifu dhidi ya ubinadamu, ukatili wa watoto, ulaghai na utakatishaji fedha.

Mwendesha mashtaka Peter Kiprop alisema wiki iliyopita kwamba kulikuwa na "taarifa za kuaminika" zinazohusisha miili iliyopatikana msituni na vifo vya "wafuasi kadhaa wasio na hatia na walio hatarini." wa Odero.

Odero na Nthenge wanashiriki "historia ya uwekezaji wa biashara" ikiwa ni pamoja na kituo cha televisheni ambacho kilitumiwa kupitisha "ujumbe mkali" kwa wafuasi, Kiprop alisema katika nyaraka za mahakama.

Wachungaji hao wawili ambao bado hawajatoa maoni yao hadharani wako kizuizini kwa sasa. Wanatarajiwa kufikishwa katika mahakama katika miji tofauti siku ya Jumanne.

TRT Afrika na mashirika ya habari