Raila Odinga, African Union (AU) High Representative for Infrastructure Development in Africa, attends an interview with Reuters in Nairobi

Polisi nchini Kenya wako katika hali ya tahadhari huku kiongozi wa upinzani nchini humo Raila Odinga akisema maandamano dhidi ya serikali ya Rais William Ruto kuhusu gharama ya juu ya maisha yataendelea.

Katika chapisho la Twitter, Odinga aliitisha maandamano kila Jumatatu na Alhamisi licha ya marufuku ya polisi.

Ilichapishwa saa chache baada ya Odinga kumshutumu Naibu Rais Rigathi Gachagua kwa kuandaa "kampeni ya ghasia" dhidi ya maandamano yaliyo pangwa.

Wiki iliyopita, jiji kuu la Nairobi lilizimwa baada ya maandamano kuwa ghasia.

Mwanafunzi wa chuo kikuu aliuawa katika mvutano kati ya waandamanaji na polisi wa kutuliza ghasia, huku maafisa 31 wakijeruhiwa.

Haki ya kupinga Siku ya Jumatatu, ulinzi ulikuwa mkali, huku polisi wa kutuliza ghasia wakiwa katika maeneo ya kimkakati jiji kuu la Nairobi, huku maduka, huduma za umma na huduma za treni zikifungwa.

Mchambuzi wa masuala ya kisiasa, Martin Ambati, alisema haki ya kuandamana ni haki ya kila Mkenya kwa mujibu wa katiba.

‘’ Inspekta Jenerali hana mamlaka na hawezi nyanganya mamlaka iliyotolewa na katiba. Hawezi kuwa mkuu kuliko katiba,” Ambati aliiambia TRT Afrika.

Idadi kubwa ya watu nchini Kenya wanakabiliwa na matatizo ya kujipatia chakula wao na familia zao kutokana na gharama kubwa ya vitu muhimu, kupungua kwa thamani ya sarafu ya nchi hiyo, na ukame mkubwa uliosababisha mamilioni ya watu kukabiliwa na njaa.

TRT Afrika