Mashirika ya ndege yanakabiliana na ongezeko la bei ya mafuta baada ya vita kati ya Marekani-Israel dhidi ya Iran kusababisha uhaba wa mafuta.
Afrika ni miongoni mwa maeneo yaliyoathirika zaidi kutokana na athari za kusitishwa kwa usambazaji na kuongezeka kwa bei.
Takriban asilimia 70 ya mafuta ya ndege yanayoagizwa kutoka nje yanapitia Mlango Bahari wa Hormuz, kwa mujibu wa shirika la uchambuzi wa masuala ya kifedha la S&P Global.
Tangu kuanza kwa mgogoro huo mwishoni mwa mwezi wa Februari, usafirishaji wa mafuta kutoka Mashariki ya Kati kupitia Mlango Bahari wa Hormuz umekaribia kusitishwa kabisa, na kusababisha uhaba wa mafuta na gesi katika soko la dunia.
"Unafika katika viwanja vya ndege Kusini, Magharibi na Afrika Mashariki na unajali bei unapofika," Jannie de Klerk, mkurugenzi mtendaji wa Shirika la Ndege la Taifa la Afrika Kusini, biashara ya ndege ambayo pia inajumuisha ndege za kusafirishia wagonjwa, ameiambia Reuters.












