| swahili
AFRIKA
2 dk kusoma
Tanzania huenda ikakabiliwa na changamoto kupata mikopo kutoka nje, amesema Rais Samia
Uwezo wa Tanzania kupata mikopo kutoka taasisi za kimataifa huenda ukakumbana na changamoto baada ya sifa yake kuharibika kimataifa, amesema Rais Samia Suluhu Hassan siku ya Jumanne wakati wa kuwaapisha mawaziri.
Tanzania huenda ikakabiliwa na changamoto kupata mikopo kutoka nje, amesema Rais Samia
Makundi ya kutetea haki za binadamu, yamesema kwamba mamia ya watu huenda waliuawa katika machafuko ya baada ya uchaguzi. @ikulu_Tanzania/
tokea masaa 11

Rais Samia, mwenye umri wa miaka 65, ambaye alitangazwa mshindi kwa asilimia 98 ya kura katika uchaguzi wa Oktoba uliogubikwa na machafuko kati ya raia na vikosi vya usalama, hakufafanua kilichosababisha kuharibika kwa sifa ya Tanzania.

Makundi ya kutetea haki za binadamu, vyama vya upinzani na Umoja wa Mataifa wamesema kwamba mamia ya watu huenda waliuawa katika machafuko hayo, ingawa serikali inakanusha takwimu hizo na kusema si za kweli.

“Mara nyingi tunategemea kupata kutoka nje: mikopo kutoka taasisi mbalimbali za kimataifa, mabenki ya kimataifa, lakini yaliotokea nchini kwetu yametutia doa kidogo,” alisema Rais Samia.

, kwa hiyo huenda yakatupunguzia sifa ya kupata hiyo mikopo kwa urahisi kama tulivyopata muhula wa kwanza wa awamu hii

“Kwa hiyo huenda yakatupunguzia sifa ya kupata mikopo hiyo kwa urahisi kama tulivyopata katika muhula wetu wa kwanza wa awamu hii… sifa mbaya tuliyojijengea inaweza kuturudisha nyuma.”

Wachunguzi wa Umoja wa Afrika walisema uchaguzi huo haukuwa wa kuaminika na walithibitisha kuwepo kwa uhalifu wa kujazwa masanduku ya kura. Serikali imepinga ukosoaji huo na kusisitiza kuwa uchaguzi ulikuwa huru na wa haki.

 Rais Samia ameahidi kuchunguza vurugu za uchaguzi na wiki iliyopita alitoa rambirambi kwa familia zilizopoteza wapendwa wao, na hivyo kuwa tamko lake la wazi zaidi kuhusu machafuko hayo ambayo yamesababisha mgogoro mkubwa zaidi wa kisiasa nchini kwa miongo kadhaa.

Wakati wa kuwaapisha mawaziri katika mji mkuu wa Dodoma siku ya Jumanne, aliwasisitiza viongozi kuelekeza nguvu zaidi katika kukusanya mapato kutoka vyanzo vya ndani.

Mwezi Juni, wizara ya fedha ilisema inapanga kukopa kiasi cha shilingi trilioni 8.7 kutoka nje katika mwaka wa fedha 2025/26 (Julai–Juni). Katika bajeti yake ya 2024/25, serikali iliweka makadirio ya kupata ruzuku na mikopo nafuu ya nje yenye thamani ya shilingi trilioni 5.13.

 

CHANZO:Reuters
Soma zaidi
Rais wa Sudan Kusini Kiir amrejesha makamu wa rais katika mabadiliko ya baraza la mawaziri
Zaidi ya watu 100,000 wamekimbia makazi yao kutoka Al Fasher ya Sudan tangu kutwaliwa na RSF
Rais wa Tanzania amteua binti na mkwe wake katika Baraza la Mawaziri
Rais Samia amteua waziri mpya wa fedha, awaacha mawaziri wa mambo ya nje na madini madarakani
Tovuti za taasisi za serikali ya Kenya zashambuliwa
Mgodi waporomoka DRC na kuua watu wasiopungua 32
Wahamiaji 4 wafariki baada ya boti mbili zilizokuwa zimebeba makumi ya watu kuzama pwani ya Libya
Kikundi cha matabibu kinaripoti visa ya ubakaji wa wasichana wa Al Fasher baada ya RSF kuteka
Mlipuko wa virusi vya Marburg umethibitishwa kusini mwa Ethiopia
DR Congo, M23 wasaini makubaliano ya amani 'ya kihistoria' nchini Qatar
Baraza la Maaskofu Tanzania lataka uwajibikaji kwa waliohusika na mauaji ya waandamanaji
Baraza la usalama la UN laongezea mwaka mmoja ujumbe wa amani wa Abyei
Kiongozi wa zamani wa waasi wa DRC anayeshtakiwa Paris kwa uhalifu wa kivita aanza mgomo wa kula
UN yaagiza uchunguzi wa dharura ufanyike kuhusu ukiukaji wa sheria katika Al Fasher ya Sudan
Rais wa Tanzania atangaza uchunguzi kuhusu mauaji ya waandamanaji katika uchaguzi
Wakimbizi 57,000 wamewasili kaskazini mwa Sudan baada ya mashambulizi ya RSF huko Darfur, Kordofan
Afrika Kusini yaruhusu kuingia kwa wakimbizi zaidi ya 150 kutoka Gaza, Palestina
Afrika yakumbwa na mlipuko wa kipindupindu mbaya zaidi katika miaka 25
Mataifa ya G7 walaani mashambulizi ya RSF dhidi ya raia Sudan, watoa wito wa kusitishwa mapigano
Wakenya zaidi ya 200 wajiunga na jeshi la Urusi