AFRIKA
1 dk kusoma
Huduma za Intaneti zarejea tena nchini Tanzania
Samia Suluhu Hassan alitangazwa mshindi katika uchaguzi wa urais wa Tanzania na kupata muhula mwingine licha ya ghasia zilizoshuhudiwa nchini humu.
Huduma za Intaneti zarejea tena nchini Tanzania
Huduma za intaneti na mawasiliano mengine uliathirika nchini Tanzania, siku ya Oktoba 29, 2025./Picha:Wengine
tokea masaa 9

Baada ya siku kadhaa za kukosekana kwa mitandao nchini Tanzania, huduma hizo zimerejea saa chache baada ya kuapishwa kwa Rais Samia Suluhu Hassan, Jumatatu ya Novemba 3, 2025.

Huduma hizo zilizitishwa kufuatia kuibuka kwa vurugu na maandamano yaliyozuka sehemu mbali mbali za nchi hiyo wakati wa Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 29.

Watu kadhaa wanahofiwa kupoteza maisha na wengine kujeruhiwa, huku mali na miundombinu ikiharibiwa wakati wa vurugu wa za baada ya uchaguzi huo.

Samia Suluhu Hassan alitangazwa mshindi katika uchaguzi wa urais wa Tanzania na kupata muhula mwingine licha ya ghasia zilizoshuhudiwa nchini humo.

Samia alipata asilimia 98 ya kura katika uchaguzi huo, kulingana na Tume Huru ya Uchaguzi nchini Tanzania INEC.

CHANZO:TRT Afrika Swahili