| Swahili
UTURUKI
2 dk kusoma
Kikao cha mwisho cha Jukwaa la Biashara kati ya Uturuki na Misri chafunguliwa jijini Cairo
Rais wa Uturuki, Recep Tayyip Erdogan, na Rais wa Misri, Abdel Fattah el Sisi, wanatarajiwa kuhudhuria kikao cha kufunga cha jukwaa hilo.
Kikao cha mwisho cha Jukwaa la Biashara kati ya Uturuki na Misri chafunguliwa jijini Cairo
Erdogan na Sisi wameweka lengo la kufikia kiwango cha biashara baina ya nchi hizo mbili cha dola bilioni 15 ifikapo 2028. / / AA
tokea masaa 7

Kikao cha kufunga cha Jukwaa la Biashara la Uturuki–Misri kilianza Cairo siku ya Jumatano, wakati Rais wa Uturuki Recep Tayyip Erdogan alipowasili katika mji mkuu wa Misri kwa ziara rasmi nchini humo.

Rais wa Uturuki aliwasili Cairo mapema Jumatano, ambako alipokelewa na mwenzake wa Misri, Abdel Fattah el Sisi.

Kituo cha habari cha serikali ya Misri, Extra News, kilisema kuwa kikao cha kufunga cha jukwaa hilo kilishuhudia “ushiriki mpana wa jumuiya za wafanyabiashara kutoka Misri na Uturuki pamoja na taasisi za kifedha na kiuchumi kutoka nchi zote mbili.”

Kwa mujibu wa kituo hicho, kikao hicho kitajadili “fursa za uwekezaji wa pamoja, kuongeza kiwango cha biashara kati ya nchi hizo mbili, kusaini mikataba mipya ya kibiashara, pamoja na kuunga mkono ushirikiano kati ya sekta binafsi za nchi hizo.”

Erdogan na Sisi wanatarajiwa kushiriki katika kikao cha kufunga cha jukwaa hilo baadaye siku ya leo, kituo hicho cha habari kiliongeza.

Kikao cha kwanza cha jukwaa hilo kilifanyika mapema Februari katika mji wa El Alamein, uliopo katika Pwani ya Kaskazini ya Misri.

Jukwaa hilo linachukuliwa kuwa moja ya mikutano mikubwa zaidi ya kibiashara kuwahi kufanyika kati ya Misri na Uturuki, likihusisha takribani wakurugenzi na maafisa 200 kutoka sekta za biashara, viwanda na masoko ya hisa ya Uturuki, pamoja na zaidi ya wawakilishi 100 wa wafanyabiashara kutoka Misri.

Mahusiano kati ya Uturuki na Misri yameonyesha kasi kubwa katika miaka ya hivi karibuni, huku kiwango cha biashara kati ya nchi hizo kikiongezeka kwa haraka.

Ziara na mawasiliano ya ngazi ya juu kati ya pande hizo mbili hivi karibuni yamesababisha kuanzishwa kwa miradi kadhaa ya pamoja katika sekta za biashara, nishati, ulinzi, utalii, afya, teknolojia na kilimo.

Kiwango cha biashara kati ya Uturuki na Misri, ambayo ni mshirika mkubwa zaidi wa kibiashara wa Uturuki barani Afrika, kilifikia dola bilioni 8.8 za Marekani mwaka 2024. Mauzo ya Uturuki kwenda Misri yalifikia dola bilioni 4.2, huku uagizaji kutoka Misri ukifikia dola bilioni 4.6.

Erdogan na Sisi wameweka lengo la kufikia kiwango cha biashara cha dola bilioni 15 kati ya nchi hizo mbili ifikapo mwaka 2028.

Ili kufanikisha lengo hilo, wizara husika katika nchi zote mbili zinaongeza juhudi kupitia mikutano mbalimbali inayolenga kuandaa mipango ya vitendo ya kuboresha mazingira ya uwekezaji ili kuunga mkono dhamira hiyo.

CHANZO:AA