| swahili
AFRIKA
1 dk kusoma
Arsenal kusitisha ushirikiano wake na Visit Rwanda
Baada ya miaka nane ya nembo ya Visit Rwanda kupamba bega la jezi za Arsenal, klabu hiyo ilitangaza kuwa itasitisha mkataba wa udhamini na Visit Rwanda ifikapo mwezi Juni 2026.
Arsenal kusitisha ushirikiano wake na Visit Rwanda
Licha ya shinikizo hizi, pande zote mbili zilikanusha kuwa sababu za kisiasa ndizo zilizopelekea kusitishwa kwa mkataba. @Arsenal /
tokea masaa 16

Hata hivyo, ushirikiano huu haukupita bila changamoto. Makundi ya haki za binadamu yalieleza wasiwasi kuhusu kuhusishwa kwa serikali ya Rwanda na kundi la M23 linalopigana dhidi ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo kwa madai. Madai ambayo Rwanda inaendelea kuyakataa.

Haya yanajiri baada ya kundi la M23 na serikali ya DRC kukubali kusitisha mapigano mapema wiki hii.

Licha ya shinikizo hizi, pande zote mbili zilikanusha kuwa sababu za kisiasa ndizo zilizopelekea kusitishwa kwa mkataba.

Katika taarifa, Arsenal ilikiri mchango mkubwa wa ushirikiano huo. Msemaji wa klabu alisema, “Uhusiano wetu na Visit Rwanda umekuwa sehemu muhimu ya mkakati wetu wa kibiashara kimataifa. Tumefanikiwa kufanya mambo makubwa pamoja, kuanzia programu za kijamii hadi kuongezea mwonekano wa Rwanda duniani.”

Kwa upande wa Rwanda, mafanikio ya ushirikiano huo yalisisitizwa pia. Mwakilishi wa Bodi ya Maendeleo ya Rwanda alisema, “Tulipoanza safari hii, lengo letu lilikuwa kuutambulisha utalii wa Rwanda kwa dunia. Kilichopatikana katika ushirikiano huu, ongezeko la watalii, kutambulika kimataifa, na ushirikiano wa kitamaduni — kilizidi matarajio yetu. Tunashukuru Arsenal kwa miaka nane yenye mafanikio.”

CHANZO:TRT Afrika
Soma zaidi
Bassirou Diomaye Faye: Rais wa Senegal
Wataalamu wa Afrika watoa wito wa kukaguliwa tathmini ya viwango vya mikopo kwa bara
Eswatini yapokea dola milioni 5.1 kupokea wahamiaji waliofurushwa Marekani, waziri anasema
Gabon yatia saini makubaliano ya kihistoria ya ufadhili wa hali ya hewa kwa misitu ya mvua ya Congo
Wanajeshi wa RSF wameripotiwa kupata hasara kubwa katika jimbo la Kordofan Kaskazini nchini Sudan
CAF yatangaza wasimamizi maarufu wa sherehe ya Tuzo za CAF 2025
Jeshi la Somalia limewauwa magaidi 11 wa Al Shabab na kuzuia shambulio la kujitoa muhanga
Tanzania huenda ikakabiliwa na changamoto kupata mikopo kutoka nje, amesema Rais Samia
Sura mpya Baraza la Mawaziri Tanzania
Cape Verde, Mauritius na Ushelisheli wafanikiwa kuangamiza surua na  rubela
Rais wa Sudan Kusini Kiir amrejesha makamu wa rais katika mabadiliko ya baraza la mawaziri
Zaidi ya watu 100,000 wamekimbia makazi yao kutoka Al Fasher ya Sudan tangu kutwaliwa na RSF
Rais wa Tanzania amteua binti na mkwe wake katika Baraza la Mawaziri
Rais Samia amteua waziri mpya wa fedha, awaacha mawaziri wa mambo ya nje na madini madarakani
Tovuti za taasisi za serikali ya Kenya zashambuliwa
Mgodi waporomoka DRC na kuua watu wasiopungua 32
Wahamiaji 4 wafariki baada ya boti mbili zilizokuwa zimebeba makumi ya watu kuzama pwani ya Libya
Kikundi cha matabibu kinaripoti visa ya ubakaji wa wasichana wa Al Fasher baada ya RSF kuteka
Mlipuko wa virusi vya Marburg umethibitishwa kusini mwa Ethiopia
DR Congo, M23 wasaini makubaliano ya amani 'ya kihistoria' nchini Qatar