| Swahili
AFRIKA
1 dk kusoma
Sudan yaanza ukarabati wa gridi ya taifa ya umeme mjini Khartoum
Khartoum imepata athari kubwa ya vita nchini Sudan, ambapo mapigano makali yameharibu vituo vya umeme.
Sudan yaanza ukarabati wa gridi ya taifa ya umeme mjini Khartoum
Jopo la wahandisi linatakiwa kuanza kazi haraka, ikiwemo kubadilisha vinu vilivyoharibiwa. / Reuters
tokea masaa 19

Sudan imepokea shehena wa kwanza wa vifaa vya ujenzi wa umeme katika Jimbo la Khartoum, hii ikiwa ni ishara ya kuanza kwa juhudi za kurejesha umeme katika mji mkuu ambao miundombinu yake iliharibiwa kutokana na vita, ripoti za Shirika la Habari la Sudan (SUNA) zinasema.

Kampuni ya Umeme ya Sudan ilitangaza kuwasili kwa vinu 400 vya umeme vyenye uwezo tofauti, vilivyotengwa mahsusi kwa ajili ya kurekebisha mtandao wa gridi ya taifa mjini Khartoum.

Kwa mujibu wa Baraza la Uratibu wa Vyombo vya Habari la kampuni, uwasilishaji huo unaashiria uzinduzi mkubwa wa mpango wa ujenzi upya wa mji mkuu.