| Swahili
UTURUKI
2 dk kusoma
Waziri wa Mambo ya Nje wa Uturuki akutana na Balozi wa Marekani Barrack, kujadili yanayojiri Syria
Mazungumzo haya yanakuja wakati Marekani inaashiria kuunga mkono makubaliano mapya yaliyotangazwa ya kusitisha mapigano na ujumuishaji kamili wa Syria, yanayolenga kurejesha eneo la kaskazini-mashariki mwa Syria chini ya udhibiti wa serikali kuu.
Waziri wa Mambo ya Nje wa Uturuki akutana na Balozi wa Marekani Barrack, kujadili yanayojiri Syria
Picha ya mkutano huo iliwekwa na Wizara ya Mambo ya Nje ya Uturuki kwenye mtandao wa kijamii wa X, bila maelezo zaidi. / / AA
20 Januari 2026

Waziri wa Mambo ya Nje wa Uturuki, Hakan Fidan, siku ya Jumanne alimpokea Balozi wa Marekani nchini Uturuki, Tom Barrack, ambaye pia ni mjumbe maalum wa Syria.

Picha ya mkutano huo iliwekwa na Wizara ya Mambo ya Nje ya Uturuki kupitia mtandao wa kijamii wa X, bila ya kutoa maelezo zaidi.

Barrack alinukuu chapisho hilo hilo na kusema: “Kuendelea na mazungumzo na Waziri wa Mambo ya Nje Hakan Fidan leo. 

Marekani ilikuwa imepongeza makubaliano mapya ya kusitisha mapigano na ya ujumuishaji kati ya serikali ya Syria na YPG siku ya Jumapili. “Makubaliano haya na usitishaji wa mapigano yanawakilisha hatua muhimu ya mabadiliko,” Barrack alisema kwenye X.

Alisema Rais wa Syria, Ahmed al Sharaa, amemthibitishia kuwa Wakurdi ni sehemu muhimu ya Syria, akiongeza: “Marekani inatazamia mchakato wa ujuimishaji utimie kwa mshirika wetu wa kihistoria katika mapambano dhidi ya Daesh.”

“Hatua ngumu ya kukamilisha maelezo ya makubaliano ya kina ya muungano inaanza sasa, na Marekani inasimama imara kuunga mkono mchakato huu katika kila hatua,” alisema.

Al Sharaa alitangaza siku ya Jumapili usitishaji kamili wa mapigano na makubaliano ya ujumuishaji kikamilifu kati ya serikali ya Syria na YPG, akieleza hatua pana za kurejesha mamlaka ya dola katika eneo la kaskazini-mashariki mwa nchi.

Kwa mujibu wa masharti yaliyochapishwa na Shirika la Habari la SANA, makubaliano hayo yanatoa wito wa kusitishwa mara moja kwa mapigano katika nyanja zote na maeneo yote ya mawasiliano kati ya majeshi ya serikali na YPG.

Makubaliano hayo yanatarajiwa kuanza kutekelezwa sambamba na kuondolewa kwa vikosi vyote vya kijeshi vinavyohusishwa na YPG kuelekea maeneo ya mashariki mwa Mto Furat, kama hatua ya maandalizi kwa ajili ya kupanga upya vikosi.

CHANZO:AA
Soma zaidi
Rais wa Uturuki awasili Ethiopia kwa ziara rasmi
Emine Erdogan awatuza wasukuma mabadiliko wakati wa makala ya 7 ya tuzo za TRT World
Rais wa Uturuki aelekea Ethiopia kwa ziara ya kikazi
Waziri Mkuu wa Somalia apongeza uchimbaji mafuta wa 'kihistoria' baharini na Uturuki
Uturuki inapanua utaalam wa reli, kutoa mafunzo kwa wafanyakazi Afrika, Asia
Erdogan: Uturuki inaendelea kutafuta amani ya kanda licha hofu iliyopo ulimwenguni
Rais wa Uturuki ateuwa Waziri mpya wa Katiba na Mambo ya Ndani katika mabadiliko ya Baraza la Mawazi
Fidan wa Uturuki akataa mashambulizi ya anga kama njia ya kubadilisha uongozi wa Iran
Makamu wa Rais wa Uturuki akutana na balozi wa Brazil
Idadi ya watu nchini Uturuki yafikia milioni 86 kwa mwaka 2025
Uturuki yalaani shambulizi la RSF nchini Sudan
Matetemeko ya ardhi ya Uturuki 2023 yalisababisha hasara ya dola bilioni 250: Erdogan
Fidan wa Uturuki akutana na Kamishna wa Maswala ya Wanachama wa EU, kujadili masuala ya ushirikiano
Rais wa Uturuki aadhimisha kumbukumbu ya miaka 3 ya tetemeko la ardhi
Uturuki imelaani shambulizi la kigaidi nchini Nigeria lililoua takriban watu 170
Uturuki kuimarisha uwepo wake wa kijeshi kuisaidia Somalia kupambana na ugaidi
Uturuki na Saudi Arabia kuimarisha ushirikiano wa ulinzi na uwekezaji katika ndege za kivita za KAAN
Mke wa Rais wa Uturuki amekutana na mwenzake wa Misri jijini Cairo
Erdogan na Sisi waimarisha ushirikiano kati ya Uturuki na Misri wajadili Gaza na migogoro ya kikanda
Kikao cha mwisho cha Jukwaa la Biashara kati ya Uturuki na Misri chafunguliwa jijini Cairo