| swahili
AFRIKA
3 DK KUSOMA
Wafahamu  watunzi wa wimbo rasmi wa AFCON 2023
Waandaaji  wa Michuano hiyo mikubwa wamefanikiwa kuleta burudani mujarab ikiwa ni sehemu ya kufurahia asili ya Afrika na soka maridhawa.
Wafahamu  watunzi wa wimbo rasmi wa AFCON 2023
Baadhi ya wanamuziki nyota Afrika walioshiriki kutunga wimbo maalumu wa AFCON 2023, maarufu kama  "Akwaba"./ Picha  Danny Synthe.
16 Januari 2024

Maoni chanya yametawala ufunguzi wa AFCON 2023, huku Rais wa CAF Patrice Motsepe akiita ''tamasha linalounganisha Afrika nzima.''

Kwa upande wake Yemi Alade mwanamuziki maarufu kutoka Nigeria, ambaye pia ameshiriki kwenye wimbo huo amelielezea tukio hilo kama 'ndoto iliyotimia.'

“Toka 2016, nilitamani kujiona nikitumbuiza kwenye matukio makubwa yanahusu soka, nikizungukwa na mamia ya wachezaji na mashabiki wengine.

“Na leo, miaka saba baadaye natumbuiza kwenye jukwaa la AFCON, hakika ni heshima sana kwangu kwani ndoto yangu imetimia. Na huu ni mwanzo tu," alijinasibu msanii huyo kwenye ukurasa wake wa X.

Waandaaji wa michuano hiyo mikubwa wamefanikiwa kuleta burudani mujarab ikiwa ni sehemu ya kufurahia asili ya Afrika na soka maridhawa.

Hata maandalizi kuelekea tamasha la ufunguzi wa michuano hiyo, yalipata idadi kubwa ya wafuatiliaji kwenye mitandao ya kijamii, huku Mohamed Ramadan msanii kutoka Misri, akiweka wazi kuwa akaunti yake ya You Tube ilivuka watazamaji bilioni 500.

Msanii huyo pia alishiriki kwenye wimbo huo, 'Akwaba', akiwa na Yemi Alade.

"Akwaba", ikimaanisha karibu kwa lugha ya Baoulé, ndio wimbo rasmi wa michuano hii, ukiwa umetungwa na kikundi cha Magic System kutoka Ivory Coast na kuzalishwa na mshindi wa tuzo za Grammy na Mwanamuziki kutoka Congo, Danny Synthe.

‘’Africa iko tayari,’’ aliandika Ramadan kwenye ukurasa wake wa Facebook, huku akiwashukuru mashabiki kwa uchangamfu waliouonyesha wakati wa ufunguzi wa AFCON 2023.

Hadi sasa, wimbo wa Akwaba umejikusanyia watazamaji zaidi ya milioni tano kwenye ukurasa wa You Tube.

Kwa mujibu wa Universal Music Africa(UMA), kampuni ya kuzalisha muziki barani Afrika, bado zipo nyingi zenye maudhui ya AFCON ambazo hazijawekwa hadharani.

‘’Ili kuongeza nakshi kwenye michuano hii, tumeleta pamoja wasanii 15 wenye vipaji, na wengine saba ambao wamebobea katika kutengeneza mirindimo, itakayowapa burudani stahiki Waafrika wote,’’ iliandika UMA kwenye ukurasa wake wa Instagram.

Mwezi uliopita, idadi ya nyimbo zenye kuzungumzia AFCON 2023 ziliwekwa kwenye mitandao kadhaa.

Walioshirikishwa kwenye nyimbo hizo ni kama vile Serge Beynaud, Kerozen na Josey.

CHANZO:TRT Afrika
Soma zaidi
UN yaagiza uchunguzi wa dharura ufanyike kuhusu ukiukaji wa sheria katika Al Fasher ya Sudan
Rais wa Tanzania atangaza uchunguzi kuhusu mauaji ya waandamanaji katika uchaguzi
Wakimbizi 57,000 wamewasili kaskazini mwa Sudan baada ya mashambulizi ya RSF huko Darfur, Kordofan
Afrika Kusini yaruhusu kuingia kwa wakimbizi zaidi ya 150 kutoka Gaza, Palestina
Afrika yakumbwa na mlipuko wa kipindupindu mbaya zaidi katika miaka 25
Mataifa ya G7 walaani mashambulizi ya RSF dhidi ya raia Sudan, watoa wito wa kusitishwa mapigano
Wakenya zaidi ya 200 wajiunga na jeshi la Urusi
AU yakanusha tuhuma za Trump kuhusu mauaji ya halaiki Nigeria
Mwigulu Nchemba ateuliwa Waziri Mkuu Tanzania
Jaji Mkenya achaguliwa Mahakama ya Kimataifa ya Haki
Rais Salva Kiir wa Sudan Kusini amfuta kazi makamu wake
Duma wa Botswana aipa India zawadi ya duma 8
Kesi ya Roger Lumbala wa DRC yaanza kusikilizwa
Kesi za ubakaji, watoto kupotea zaripotiwa Darfur, Sudan – Umoja wa Mataifa
Ugonjwa wa Kichaa cha mbwa barani Afrika: Janga linaloendelea kuathiri maisha japo linaepukika
Libya yatakiwa kufunga vituo vya kuwazuilia wahamiaji katika mkutano wa Umoja wa Mataifa
Rais Museveni aonya kuzuka kwa vita endapo nchi za Afrika zitashindwa kufikia Bahari ya Hindi
UN: Milioni 11 wanawake na wasichana wanabeba uzito mkubwa wakati njaa ya Sudan inaendelea kupamba moto
Ethiopia yachagguliwa kuwa mwenyeji wa mkutano wa Umoja wa Mataifa kuhusu hali ya hewa, COP32
Ghana yafichua sababu ya ajali ya helikopta iliyoua watu wanane, wakiwemo mawaziri, mwezi Agosti