| swahili
AFRIKA
3 DK KUSOMA
Walimu Uganda sharti kuwa na shahada ya kwanza
Serikali ya Uganda inapendekeza walimu wote nchini humo kuwa na shahada ya kwanza kama kiwango cha chini zaidi. Mwanasheria Mkuu amesema walimu ambao watashindwa kupata sifa hizo ndani ya miaka 10 baada ya sera hiyo kupitishwa wataondolewa.
Walimu Uganda sharti kuwa na shahada ya kwanza
Muswada wa Sheria ya Taifa ya Walimu wa mwaka 2024 unapendekeza walimu wote wawe na shahada ya kwanza kabla ya kuajiriwa/ picha kutoka Wizara ya Elimu na Michezo Uganda 
20 Novemba 2024

Mwanasheria Mkuu wa Serikali ya Uganda Kiwanuka Kiryowa ametetea hitaji la walimu wote nchini humo kuwa na shahada ya kwanza kama hitaji la msingi kupata ajira.

"Nadhani kwa tathmini ambayo imetolewa na kufanywa na Serikali, hatukosi watu wenye kiwango hiki cha elimu. Sheria hii ilipotungwa tulikuwa hatuna haja walimu kuwa na shahada, sasa tunayo," Kiryowa ameiambia Kamati ya Bunge.

Alikuwa akijibu hoja zilizotolewa na wadau mbalimbali kuhusu Muswada wa Sheria ya Taifa ya Walimu ya mwaka 2024.

Irene Linda Mugisha mbunge wa wanawake wa mji wa Fort Portal alishangaa kwa nini Serikali ambayo haijawekeza au kumiliki shule za awali,au chekechea baada ya kuiachia sekta binafsi inadai walimu wa shule za chekekea wawe na shahada ya kwanza kama kiwango cha chini.

“Tunaweka kiwango cha Shahada ya Kwanza, hivi hizi taasisi binafsi zitalipa kiasi gani cha fedha? Hii ina maana kwamba, tunakwenda kuhamisha gharama kwa wazazi kwa sababu kama serikali, kwanza tumeshindwa kuwalipa walimu wetu," Mugisha alisema.

"Ukiangalia shule za msingi tumeshindwa kuwalipa walimu wote, hadi sasa wazazi wanalipa walimu kwa hiyo sasa tunasema hata kwa shule ya awali wawe na shahada ya kwanza na bado Serikali tumeshindwa kumiliki shule hizo. Shule hizi za awali, zinamilikiwa na taasisi binafsi. Kwa hivyo, hufikirii kwamba tunaenda kwa bidii kidogo?" Mugisha alimuuliza Mwanasheria Mkuu wa Serikali.

Mugisha alishangaa ni kwa nini Serikali haizingatii fursa ya kuanzisha malipo ya kitaaluma ili kuwapa motisha walimu hao ili wapandishe sifa zao za elimu. Kwa mfano, kuhakikisha kuwa mwalimu akipata shahada ya kwanza, atalipwa moja kwa moja zaidi ili kuwawezesha walimu hao kupandisha madaraja yao taratibu badala ya kuwalazimisha.

Lakini Mwanasheria Mkuu wa Serikali alisisitiza kuwa uamuzi wa serikali unawakilisha matarajio ya wananchi.

“Sheria hizi zinazungumzia matarajio ya watu wa Uganda, tunatamani kuona nini? Na tunachotamani kuona ni mfumo wa elimu ambao kwa hakika ni mahiri na unaojali mahitaji ya wanafunzi na pia walimu. Lakini matarajio yetu ni kuwa na watu wa elimu ya awali wanaosomeshwa na watu wenye shahada na sifa zinazohitajika kama zitakavyowekwa mara kwa mara na Baraza kwa kushauriana na Serikali,” alifafanua Kiryowa.

Amesema watu ambao wako serikalini sasa, lazima wafanye kazi ya kubadilisha mfumo wa mahitaji ya walimu. Wamepewa muda wa miaka 10 wa mpito wa kutimiza haya.

Amesema ikiwa hawatabadilika kwa miaka 10 na sheria ikabaki kama ilivyo, wataondolewa kwa sababu watu walio na shahada ya kwanza wataingia katika soko la ajira.

CHANZO:TRT Afrika
Soma zaidi
UN yaagiza uchunguzi wa dharura ufanyike kuhusu ukiukaji wa sheria katika Al Fasher ya Sudan
Rais wa Tanzania atangaza uchunguzi kuhusu mauaji ya waandamanaji katika uchaguzi
Wakimbizi 57,000 wamewasili kaskazini mwa Sudan baada ya mashambulizi ya RSF huko Darfur, Kordofan
Afrika Kusini yaruhusu kuingia kwa wakimbizi zaidi ya 150 kutoka Gaza, Palestina
Afrika yakumbwa na mlipuko wa kipindupindu mbaya zaidi katika miaka 25
Mataifa ya G7 walaani mashambulizi ya RSF dhidi ya raia Sudan, watoa wito wa kusitishwa mapigano
Wakenya zaidi ya 200 wajiunga na jeshi la Urusi
AU yakanusha tuhuma za Trump kuhusu mauaji ya halaiki Nigeria
Mwigulu Nchemba ateuliwa Waziri Mkuu Tanzania
Jaji Mkenya achaguliwa Mahakama ya Kimataifa ya Haki
Rais Salva Kiir wa Sudan Kusini amfuta kazi makamu wake
Duma wa Botswana aipa India zawadi ya duma 8
Kesi ya Roger Lumbala wa DRC yaanza kusikilizwa
Kesi za ubakaji, watoto kupotea zaripotiwa Darfur, Sudan – Umoja wa Mataifa
Ugonjwa wa Kichaa cha mbwa barani Afrika: Janga linaloendelea kuathiri maisha japo linaepukika
Libya yatakiwa kufunga vituo vya kuwazuilia wahamiaji katika mkutano wa Umoja wa Mataifa
Rais Museveni aonya kuzuka kwa vita endapo nchi za Afrika zitashindwa kufikia Bahari ya Hindi
UN: Milioni 11 wanawake na wasichana wanabeba uzito mkubwa wakati njaa ya Sudan inaendelea kupamba moto
Ethiopia yachagguliwa kuwa mwenyeji wa mkutano wa Umoja wa Mataifa kuhusu hali ya hewa, COP32
Ghana yafichua sababu ya ajali ya helikopta iliyoua watu wanane, wakiwemo mawaziri, mwezi Agosti