| Swahili
AFRIKA
1 dk kusoma
Rais Museveni ataka serikali imiliki mtandao wa intaneti Uganda
Rais wa Uganda Yoweri Museveni amependekeza kuwa Serikali lazima iwe na mamlaka juu ya mifumo ya msingi ya mtandao ili kuhakikisha upatikanaji wa huduma hiyo kwa bei nafuu.
Rais Museveni ataka serikali imiliki mtandao wa intaneti Uganda
Rais Museveni, ambaye amekuwa madarakani tangu 1986, anagombea urais kwa muhula wa saba. / / Reuters
4 Desemba 2025

Rais wa Uganda Yoweri Museveni amesema kuwa miundombinu ya mtandao haipaswi kumilikiwa au kuendeshwa na makampuni ya binafsi, na kuongeza kusema kuwa udhibiti wa serikali ni muhimu ili kupunguza gharama za upatikanaji wa huduma hiyo kwa raia.

Akizungumza wakati wa mkutano na waandishi wa habari, Museveni alisema kuwa umiliki wa makampuni binafsi mara nyingi huongeza gharama kwani makampuni yanaendeshwa na faida badala ya maslahi ya taifa.

Kulingana na Rais Museveni, hali hiyo inafanya gharama za uunganishaji kwa raia kuwa kuwa ghali.

"Mtandao wa intaneti haupaswi kumilikiwa na watu binafsi...kwa sababu wakati mtandao unamilikiwa na wafanyabiashara, lengo lao ni kutafuta pesa, ndiyo maana unapaswa kumilikiwa na serikali."

Alibainisha kuwa wakati watoa huduma wa kibinafsi wanachukua nafasi muhimu ya kutoa huduma, hawapaswi kudhibiti njia muhimu za usambazaji.

Museveni, ambaye amekuwa madarakani tangu 1986, anagombea urais kwa muhula wa saba.

CHANZO:TRT Afrika