| swahili
AFRIKA
3 DK KUSOMA
Nchi za Afrika zatuma rambirambi kwa Uturuki baada ya ajali ya moto
Moto uliotokea kwenye sehemu ya kitalii kaskazini mwa nchi, ulisababisha vifo vya takriban watu 76 na kuwajeruhi wengine 51, Waziri wa Mambo ya Ndani wa Uturuki Ali Yerlikaya alisema Jumanne.
Nchi za Afrika zatuma rambirambi kwa Uturuki baada ya ajali ya moto
Kartalkaya, katika mkoa wa Bolu, ni mojawapo ya maeneo ya utalii ya majira ya baridi nchini Uturuki / Picha: AA
22 Januari 2025

Nchi za Afrika zimeungana na zingine duniani kutoa pole kwa Uturuki kufuatia ajali ya moto katika hoteli ya Kartalkaya Ski resort, kaskazini mwa Uturuki.

Rais wa Rwanda Paul Kagame alituma salamu zake za rambirambi kwa rais wa Uturuki.

" Rambirambi zangu za dhati kwa Rais Recep Tayyip Erdoğan na watu wa Uturuki kwa vifo vilivyotokana na moto mkali katika kituo cha utalii huko Bolu.Tunawatakia familia za waliofiwa faraja na wote walioathiriwa na msiba huu. Tunawatakia ahueni waliojeruhiwa.”

Moto uliotokea kwenye kituo cha kuteleza kwenye theluji ulisababisha vifo vya takriban watu 76 na kuwajeruhi wengine 51, Waziri wa Mambo ya Ndani wa Uturuki Ali Yerlikaya alisema Jumanne.

Kati ya waliojeruhiwa, 17 waliruhusiwa kutoka hospitali huku mmoja akisalia katika chumba cha wagonjwa mahututi, alisema Waziri wa Afya Kemal Memisoglu.

Moto huo ulizuka mwendo wa saa tisa na dakika 27 asubuhi kwa saa za Uturuki katika eneo la mgahawa wa hoteli ya Kartalkaya, na kuteketeza jengo hilo, kulingana na Gavana wa Bolu, Abdulaziz Aydin.

Ethiopia nayo imetoa ujumbe wake kupitia taarifa kutoka Wizara ya Mambo ya Nje.

" Wizara ya Mambo ya nje Ethiopia inatoa pole kwa familia za waliofiwa na kuwatakia ahueni ya haraka majeruhi wa ajali hiyo ya moto."

Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje nchini Nigeria pia amewasilisha ujumbe wa serikali yake.

" Serikali ya Nigeria inatoa rambirambi kwa serikali ya Uturuki na familia za walioathirika na ajali hiyo ya moto, na pia inawatakia ahueni ya haraka waliojeruhiwa." Kimiebi Ebienfa amesema katika taarifa.

Siku ya taifa ya maombolezo

Uturuki imetangaza siku moja ya maombolezo ya kitaifa siku ya Jumatano.

Rais Recep Tayyip Erdogan Jumanne alitoa salamu za rambirambi kwa familia za waliopoteza wapendwa wao, na kuwaombea faraja na kupona haraka kwa waliojeruhiwa.

Aliwahakikishia wananchi kuwa waliohusika na maafa hayo, iwe kwa uzembe au utovu wa nidhamu, watawajibishwa.

CHANZO:TRT Afrika
Soma zaidi
UN: Milioni 11 wanawake na wasichana wanabeba uzito mkubwa wakati njaa ya Sudan inaendelea kupamba moto
Ethiopia yachagguliwa kuwa mwenyeji wa mkutano wa Umoja wa Mataifa kuhusu hali ya hewa, COP32
Ghana yafichua sababu ya ajali ya helikopta iliyoua watu wanane, wakiwemo mawaziri, mwezi Agosti
Nigeria yaanzisha uchunguzi baada ya kukamata kilo 1,000 za kokeini yenye thamani ya $235M
Kenya kuanzisha balozi zake mpya Vatican City, Denmark na Vietnam
Mtoto wa Gaddafi aachiliwa huru baada ya miaka kumi gerezani
Kuanzia vifo vya taratibu hadi mauaji ya ukatili: Kutoweka kwa utu Al Fasher
Zaidi ya mataifa 20 yanalaani ukatili wa RSF nchini Sudan, na kutaka kukomeshwa kwa ghasia
Rais wa Misri, afisa mkuu wa usalama wa Urusi kujadili ushirikiano wa kijeshi
Maelfu ya wananchi wanashikiliwa katika hali mbaya sana katika Al Fasher, Sudan: madaktari
Makamu wa Rais wa Marekani JD Vance aghairi ziara iliyopangwa nchini Kenya
‘Mauaji ya waandamanaji ni chukizo mbele za Mungu’
Jeshi la Sudan lazima shambulio la RSF katika mji wa Babnousa huko Kordofan Magharibi
Majeshi ya Somalia yawaua viongozi watatu wakuu wa Al Shabaab
Rwanda, DRC zaanzisha mfumo wa ushirikiano wa kiuchumi huku kukiwa na mazungumzo ya amani
RSF yazika miili katika makaburi ya halaiki, inachoma wengine ili 'kuficha ushahidi wa mauaji
Wananchi katika Al Fasher, Sudan, wanakabiliwa na ukatili 'wa kiwango kisichoweza kuaminika' — UN
Chama tawala nchini Djibouti kimemteua Rais Guelleh kwa muhula wa sita
Amaan Golugwa akamatwa huku polisi Tanzania ikiwasaka viongozi wa upinzani kufuatia maandamano
Wafanyakazi waokolewa baada ya maharamia kushambulia meli ya mafuta kutoka Somalia