| Swahili
UTURUKI
2 DK KUSOMA
Uturuki iko tayari kusaidia kumaliza mgogoro wa Rwanda na DRC- Erdogan
Recep Tayyip Erdogan amepongeza jitihada za Rwanda kupambana na magaidi wa FETO
Uturuki iko tayari kusaidia kumaliza mgogoro wa Rwanda na DRC- Erdogan
Tangu mwaka 2022, kikundi cha waasi cha M23 kimeendeleza machafuko katika eneo la Mashariki mwa DRC./Picha: AA  / Others
23 Januari 2025

Uturuki iko tayari kutoa msaada wa aina yoyote kumaliza uhasama kati ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo na Rwanda, iwapo pande hizo zitahitaji msaada huo, Rais Recep Tayyip Erdogan amesema

“Sisi, kama Uturuki tuko tayari kusaidia kwa njia yoyote ile kumaliza mgogoro kati ya Rwanda na DRC, hatua ambayo itachangia kwa kiasi kikubwa upatikanaji wa amani na utulivu katika kanda ya Maziwa Makuu, iwapo tu nchi hizo zitaridhia,” alisema Erdogan siku ya Alhamisi, katika mkutano wa pamoja na waandishi wa habari akiwa na mgeni wake Rais Paul Kagame jijini Ankara.

Tangu mwaka 2022, kikundi cha waasi cha M23 kimeendeleza machafuko katika eneo la Mashariki mwa DRC.

Kinshasa na nchi zingine zimeishutumu Rwanda kwa kukisaidia kikundi hicho, tuhuma ambazo zimepingwa na Kigali.

Erdogan pia alipongeza jitihada za Rwanda za kukabiliana na shirika la kigaidi la FETO.

FETO iliongoza mapinduzi yaliyoshindwa ya Julai 15, 2016 ambayo yalisababisha vifo vya watu 252 na majeruhi 2,734 nchini Uturuki.

Uturuki inaituhumu FETO kwa kushiriki katika kampeni ya kuipindua serikali kupitia kujipenyeza ndani ya taasisi za Uturuki, hususani jeshi, polisi na mahakama.

Pata habari zaidi kupitia Whatsapp channels

CHANZO:TRT Afrika
Soma zaidi
Emine Erdogan awatuza wasukuma mabadiliko wakati wa makala ya 7 ya tuzo za TRT World
Rais wa Uturuki aelekea Ethiopia kwa ziara ya kikazi
Waziri Mkuu wa Somalia apongeza uchimbaji mafuta wa 'kihistoria' baharini na Uturuki
Uturuki inapanua utaalam wa reli, kutoa mafunzo kwa wafanyakazi Afrika, Asia
Erdogan: Uturuki inaendelea kutafuta amani ya kanda licha hofu iliyopo ulimwenguni
Rais wa Uturuki ateuwa Waziri mpya wa Katiba na Mambo ya Ndani katika mabadiliko ya Baraza la Mawazi
Fidan wa Uturuki akataa mashambulizi ya anga kama njia ya kubadilisha uongozi wa Iran
Makamu wa Rais wa Uturuki akutana na balozi wa Brazil
Idadi ya watu nchini Uturuki yafikia milioni 86 kwa mwaka 2025
Uturuki yalaani shambulizi la RSF nchini Sudan
Matetemeko ya ardhi ya Uturuki 2023 yalisababisha hasara ya dola bilioni 250: Erdogan
Fidan wa Uturuki akutana na Kamishna wa Maswala ya Wanachama wa EU, kujadili masuala ya ushirikiano
Rais wa Uturuki aadhimisha kumbukumbu ya miaka 3 ya tetemeko la ardhi
Uturuki imelaani shambulizi la kigaidi nchini Nigeria lililoua takriban watu 170
Uturuki kuimarisha uwepo wake wa kijeshi kuisaidia Somalia kupambana na ugaidi
Uturuki na Saudi Arabia kuimarisha ushirikiano wa ulinzi na uwekezaji katika ndege za kivita za KAAN
Mke wa Rais wa Uturuki amekutana na mwenzake wa Misri jijini Cairo
Erdogan na Sisi waimarisha ushirikiano kati ya Uturuki na Misri wajadili Gaza na migogoro ya kikanda
Kikao cha mwisho cha Jukwaa la Biashara kati ya Uturuki na Misri chafunguliwa jijini Cairo
Erdogan na Mwanamfalme wa Saudia waunga mkono umoja wa Somalia, wajadili masuala ya kikanda