UTURUKI
1 dk kusoma
Shirika la Ndege la Uturuki kuanza tena safari zake Sudan kwa mara ya kwanza tangu vita kuanza
Balozi wa Uturuki nchini Sudan ametangaza kuanza tena kwa safari za ndege za kampuni hiyo hadi Port Sudan.
Shirika la Ndege la Uturuki kuanza tena safari zake Sudan kwa mara ya kwanza tangu vita kuanza
Shirika la Ndege la Uturuki sasa linaruka hadi maeneo 63 kote Afrika.
18 Septemba 2025

Shirika la Ndege la Uturuki limeanza tena safari za moja kwa moja kuelekea Sudan baada ya kusitisha huduma kwa miezi 29 kutokana na vita vya wenyewe kwa wenyewe nchini humo.

Sudan imekuwa ikikumbwa na vita vya wenyewe kwa wenyewe kati ya jeshi la taifa na kikosi cha wanamgambo cha Rapid Support Forces (RSF) tangu Aprili 2023, hali ambayo imesababisha vifo vya maelfu ya watu na mamilioni kuyahama makazi yao, kulingana na mashirika ya Umoja wa Mataifa.

Balozi wa Uturuki nchini Sudan alitangaza kurejea kwa safari za shirika hilo kuelekea Port Sudan, mji mkubwa zaidi wa bandari nchini humo.

"Kwa safari hizi, Waturuki na Uturuki kwa mara nyingine wameonyesha mshikamano wao na marafiki zao katika nyakati ngumu," alisema Balozi Fatih Yildiz.

‘Kuonyesha urafiki’

"Kupitia safari hizi, tumetoa ujumbe mzito kwamba Sudan haiko peke yake, kwamba tumejizatiti kupinga wale wanaotaka kuitenga Sudan, na kwamba tumeonyesha urafiki wetu," alisema.

"Safari hizi zinaonyesha kuwa Shirika la Ndege la Uturuki ni nguzo muhimu ya sera ya kigeni na diplomasia ya Uturuki," aliongeza.

Kwa kuanzisha safari za kuelekea Port Sudan, Turkish Airlines sasa imeongeza idadi ya maeneo inayoenda barani Afrika kufikia 63.

Soma zaidi
Palestina inapongeza amri za kukamatwa dhidi ya maafisa 37 wa Israel kutoka Uturuki kama 'ushindi
Ujumbe wa Erdogan 'Azerbaijan haiko peke yake' ulipelekea ushindi wa Karabakh: Aliyev
Ushindi wa Karabakh wa Azerbaijan kwa amani ya Caucasus: Rais Erdogan
Uturuki yatoa hati ya kukamatwa kwa Waziri Mkuu wa Israel Netanyahu, juu ya mashtaka ya mauaji
Erdogan: Uturuki kuharakisha miradi ya kiulinzi kuimarisha ‘maslahi’ na washirika wa Ulaya
Uturuki kuandaa mazungumzo ya Gaza wiki ijayo kufuatia wasiwasi juu ya usitishaji mapigano – Fidan
Mfumo wa ulimwengu wa sasa unazingatia nguvu zaidi ya haki: Mkurugenzi wa TRT
Israel imeigeuza Gaza kuwa vifusi, inawezaji kuwa haina hatia: Erdogan
Uturuki yakashifu unafiki wa nchi za Magharibi kuhusu Gaza, yatoa wito wa mfumo mpya wa dunia
Hamas haina nuyklia, Israel iko nayo: Erdogan aitaka Berlin ichukue hatua kali dhidi ya Tel Aviv
Erdogan ataka kuona mabadiliko katika uhusiano na EU na ushirikiano wa kikanda alipokutana na Mertz
Ujerumani yatoa wito wa kuunda “ushirikiano wa kimkakati” ili kukabiliana na changamoto za kimataifa
"Marekebisho ya Ulimwengu": Jukwaa la 9 la TRT World kuanza Istanbul likiangazia majadiliano na haki
Erdogan ametangaza washindi wa Tuzo Kuu za Utamaduni na Sanaa za Urais mwaka 2025
Uturuki yaadhimisha miaka 102 tangu kuanzishwa kwa Jamhuri
Uturuki yatoa wito wa kusitishwa mara moja kwa mapigano katika mji wa Al Fasher, Sudan
Uturuki na Jordan zasaini makubaliano ya kuimarisha uhusiano wa kiuchumi
Erdogan atangaza kukabidhiwa kwa jeshi vifaru vya kwanza  vya Altay vilivyotengenezwa Uturuki
Israel inaishutumu 'Uturuki chini ya utawala wa Erdogan’ kuwa na uhasama mkali dhidi yake
Erdogan na Starmer wasaini mkataba wa ndege za kivita za Eurofighter Typhoon