| swahili
AFRIKA
2 dk kusoma
Mwanamfalme wa Qatar ataka kuwekeza dola bilioni 21 DRC,serikali ya nchi hiyo imesema
Mwanamfalme wa Qatar Sheikh Mansour bin Jabr bin Jassim Al Thani anataka kuwekeza dola bilioni 21 nchini DRC, serikali ya nchi hiyo ilitangaza siku ya Jumatano.
Mwanamfalme wa Qatar ataka kuwekeza dola bilioni 21 DRC,serikali ya nchi hiyo imesema
Mwanamfalme wa Qatar Sheikh Mansour bin Jabr bin Jassim Al Thani ana mpango wa kuwekeza mabilioni ya madola nchini DRC. / TRT Afrika English
3 Septemba 2025

Shirika la uwekezaji la Al Mansour Holding linatarajia kuwekeza dola bilioni 21 katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, ambapo Qatar ni mpatanishi kwa lengo la kumaliza vita vya miaka mingi mashariki mwa nchi, serikali ya DRC ilitangaza siku ya Jumatano.

Mwanzilishi wa shirika hili na mmoja wa Wanamfalme Sheikh Mansour bin Jabr bin Jassim Al Thani alifanya ziara mji mkuu wa DRC, Kinshasa siku ya Jumanne ikiwa sehemu ya ziara yake ya bara la Afrika.

Ujumbe wa Qatar uliwasilisha ‘‘mapendekezo" ya kutaka kuwekeza karibu dola bilioni 21 nchini DRC wakati wa mkutano na Waziri Mkuu Judith Suminwa, ofisi yake ilisema katika taarifa.

Uwekezaji huo utakuwa katika sekta mbalimbali, ikiwemo kilimo, fedha, uchimbaji madini, dawa na haidrokaboni, iliongeza.

Kufanya ziara 'ya kibinafsi' DRC

Shirika la habari la AFP, lilipowasiliana nao, Afisa mmoja wa Qatar alisema Sheikh Mansour alikuwa anafanya ziara ya kibinafsi DRC kama mfanyabiashara.

Mapigano katika eneo la mashariki mwa DRC kwenye utajiri mkubwa wa madini yameongezeka mapema mwaka huu baada ya waasi wa M23 kuanzisha mashambulizi, na kufanikiwa kudhibiti miji mikuu miwili ya mkoa katika kipindi cha wiki chache.

Juhudi za kidiplomasia kutafuta kumaliza mzozo huo zilikwama hadi ghafla Qatar ilipotangaza kuwa Rais wa Rwanda Paul Kagame na mwenzake wa DRC Felix Tshisekedi walikutana jijini Doha kwa mazungumzo katikati ya mwezi Machi.

Nchi hizo mbili zilitia saini makubaliano ya amani mwezi Juni jijini Washington.

Kwa upande mwingine, serikali ya DRC na M23 walianza mazungumzo Doha, mwezi Aprili, na kutangaza kusitisha vita mwezi Julai. Hata hivyo, mapigano yameendelea katika eneo hilo.

CHANZO:TRT Afrika Swahili
Soma zaidi
Kiongozi wa zamani wa waasi wa DRC anayeshtakiwa Paris kwa uhalifu wa kivita aanza mgomo wa kula
UN yaagiza uchunguzi wa dharura ufanyike kuhusu ukiukaji wa sheria katika Al Fasher ya Sudan
Rais wa Tanzania atangaza uchunguzi kuhusu mauaji ya waandamanaji katika uchaguzi
Wakimbizi 57,000 wamewasili kaskazini mwa Sudan baada ya mashambulizi ya RSF huko Darfur, Kordofan
Afrika Kusini yaruhusu kuingia kwa wakimbizi zaidi ya 150 kutoka Gaza, Palestina
Afrika yakumbwa na mlipuko wa kipindupindu mbaya zaidi katika miaka 25
Mataifa ya G7 walaani mashambulizi ya RSF dhidi ya raia Sudan, watoa wito wa kusitishwa mapigano
Wakenya zaidi ya 200 wajiunga na jeshi la Urusi
AU yakanusha tuhuma za Trump kuhusu mauaji ya halaiki Nigeria
Mwigulu Nchemba ateuliwa Waziri Mkuu Tanzania
Jaji Mkenya achaguliwa Mahakama ya Kimataifa ya Haki
Rais Salva Kiir wa Sudan Kusini amfuta kazi makamu wake
Duma wa Botswana aipa India zawadi ya duma 8
Kesi ya Roger Lumbala wa DRC yaanza kusikilizwa
Kesi za ubakaji, watoto kupotea zaripotiwa Darfur, Sudan – Umoja wa Mataifa
Ugonjwa wa Kichaa cha mbwa barani Afrika: Janga linaloendelea kuathiri maisha japo linaepukika
Libya yatakiwa kufunga vituo vya kuwazuilia wahamiaji katika mkutano wa Umoja wa Mataifa
Rais Museveni aonya kuzuka kwa vita endapo nchi za Afrika zitashindwa kufikia Bahari ya Hindi
UN: Milioni 11 wanawake na wasichana wanabeba uzito mkubwa wakati njaa ya Sudan inaendelea kupamba moto
Ethiopia yachagguliwa kuwa mwenyeji wa mkutano wa Umoja wa Mataifa kuhusu hali ya hewa, COP32