| Swahili
ULIMWENGU
2 dk kusoma
Mkuu wa Jeshi la Iran atishia kujibu 'vitisho' vya Trump na Netanyahu
Maandamano yaliyosababishwa na ugumu wa maisha nchini Iran yanafuatiliwa kwa karibu na jamii ya kimataifa, ikiwa ni pamoja na viongozi mahasimu wa taifa hilo, Israel na Marekani.
Mkuu wa Jeshi la Iran atishia kujibu 'vitisho' vya Trump na Netanyahu
Kiongozi wa kijeshi wa Iran alionya kwamba Iran haitakaa kimya, baada ya Marekani na Israel kuunga mkono maandamano dhidi ya serikali. / Reuters
7 Januari 2026

Kiongozi wa kijeshi wa Iran alionya kwamba Iran haitakaa kimya, baada ya Marekani na Israel kuunga mkono maandamano dhidi ya serikali.

"Jamhuri ya Kiislamu ya Iran inachukulia kuongezeka kwa kauli za uhasama dhidi ya taifa la Iran kuwa tishio na haitavumilia kuendelea kwake bila kujibu," alisema Jenerali Amir Hatami, kwa mujibu wa shirika la habari la Fars siku ya Jumatano.

Hatami, kamanda wa jeshi la Iran, alionya kwamba "ikiwa adui atafanya kosa" mwitikio wa Iran utakuwa mkali zaidi kuliko ule wa wakati wa vita vya siku 12 dhidi ya Israel mwezi Juni 2025.

Hivi karibuni, Rais wa Marekani Donald Trump ametishia kuingilia kati iwapo Iran itauwa waandamanaji, wakati huo huo Benjamin Netanyahu Waziri Mkuu wa Israel ameonyesha kuunga mkono maandamano hayo.

Tarehe 28 Disemba wafanyabiashara mjini Tehran walifanya maandamano kupinga ongezeko la bei na kuanguka kwa sarafu ya nchi hiyo rial, jambo lililosababisha maandamano kama hayo kufanyika katika miji kadhaa.

Maandamano hayo bado hayajakuwa makubwa kama yale ya mwaka 2022 hadi 2023, au yale ya 2009 yaliyojitokeza baada ya uchaguzi wa urais.

Lakini maandamano ya kiuchumi yamevutia jumuia ya kimataifa, ikiwemo kutoka kwa viongozi wa mataifa ambayo hayana uhusiano mzuri na Iran.

"Tunaangalia kwa makini sana. Ikiwa wataanza kuua watu kama walivyofanya zamani, nadhani watashambuliwa vikali na Marekani," Trump aliwaambia waandishi wa habari Jumapili.

Netanyahu, kwa upande mwingine, alisema mbele ya baraza la mawaziri la Israel: "Tunaungana kwa mshikamano na watu wa Iran na matarajio yao ya uhuru, uhuru binafsi na haki."

Jumatatu, Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran ilimshutumu Trump na Netanyahu kwa kuhamasisha vurugu na kujaribu kuharibu umoja wa kitaifa wa Iran.

Soma zaidi
Trump atishia shambulio la pili Venezuela, aonya kuhusu operesheni nyingine Colombia
Dunia imepokea vipi shambulio la Marekani nchini Venezuela?
Mashambulizi ya Marekani nchini Venezuela yaliua takriban watu 40: ripoti
Mwanabondia Anthony Joshua arejea Uingereza baada ya ajali ya gari Nigeria
Je, ajenda ya Marekani kubadili mfumo itafanikiwa Venezuela?
Shutuma za kimataifa zaongezeka kutokana na mashambulizi ya Marekani dhidi ya Venezuela
Rais Maduro na mkewe wamelazimika kuondoka Venezuela, anasema Trump
Milipuko yatikisa Caracas kufuatia onyo la Trump la kushambulia Venezuela
Venezuela yawaachia wafungwa 88 wa maandamano ya baada ya uchaguzi
Maelfu waandamana jijini Istanbul kuunga mkono Wapalestina
Israel inataka kufuta vibali vya mashirika ya misaada Gaza na Ukingo wa Magharibi
Watu 6 wameuawa Syria kufuatia shambulio la msikitini wakati wa swala ya Ijumaa
Papa Leo azungumzia madhila ya Gaza katika mahubiri ya Krismasi yake ya kwanza
Papa Leo aadhimisha mkesha wa Krismasi kwa mara ya kwanza kama Baba Mtakatifu
Ubelgiji yajiunga katika kesi ya mauaji ya halaiki ya Afrika Kusini dhidi ya Israel
Marekani yatoa ofa ya $3000 kwa wahamiaji kujiondoa nchini, nyongeza ya mara tatu
Trump awafuta kazi mabalozi 30 wa Marekani katika msukumo wa ajenda ya 'Amerika Kwanza'
Jenerali mwandamizi wa Urusi auawa katika shambulio la gari Moscow
Elon Musk anakuwa bilionea wa kwanza duniani wa $700b baada ya mkataba wa malipo wa Tesla kurejeshwa
Israel yashambulia kwa mabomu harusi ya Gaza na kuua Wapalestina 6 licha ya makubaliano ya amani