| Swahili
AFRIKA
2 dk kusoma
Tanzania yapiga marufuku wageni kutoa baadhi ya huduma katika sekta ya madini, kulinda wazawa
Lengo ni kupanua wigo wa ushiriki wa wazawa na kuongeza manufaa ya moja kwa moja kwa taifa.
Tanzania yapiga marufuku wageni kutoa baadhi ya huduma katika sekta ya madini, kulinda wazawa
Anthony Mavunde, Waziri wa Madini Tanzania / TRT Afrika Swahili
5 Januari 2026

Maelfu ya Watanzania wanaotegemea sekta ya madini kama chanzo kikuu cha mapato wanatarajiwa kuanza kunufaika zaidi baada ya Serikali kuanza utekelezaji rasmi wa Kanuni ya 13, inayolenga kuwalinda wazawa katika sekta hiyo.

Serikali imetangaza kufanya marekebisho ya Kanuni za Ushirikishwaji wa Watanzania za mwaka 2018, ambapo kupitia Kanuni ya 13A, Tume ya Madini itakuwa ikitangaza mara kwa mara orodha ya bidhaa na huduma zinazopaswa kutolewa na kampuni zinazomilikiwa kwa asilimia 100 na Watanzania.

Lengo ni kupanua wigo wa ushiriki wa wazawa na kuongeza manufaa ya moja kwa moja kwa taifa.

Hatua hiyo inatarajiwa kupunguza malalamiko ya muda mrefu kwamba rasilimali za madini haziwanufaishi Watanzania ipasavyo. Marufuku hiyo, iliyoanza kutekelezwa Novemba 15 mwaka jana, imetangazwa rasmi leo na Waziri wa Madini, Anthony Mavunde.

Akizungumza na vyombo vya habari Jijini Dodoma, Mavunde amesema miongoni mwa maeneo yaliyopigwa marufuku kwa wageni ni uchimbaji wa moja kwa moja, ambapo sasa utaruhusiwa tu kwa mfumo wa mkataba, pamoja na usambazaji wa jumla wa vilainishi na mafuta ya kulainisha mitambo.

“Migodi mikubwa imekuwa ikiagiza bidhaa kutoka nje, hata zile zinazopatikana nchini, hali iliyosababisha fedha nyingi kutoka nje ya nchi bila kuzinufaisha Serikali,” alisema Mavunde, akiongeza kuwa hata bidhaa za msingi kama mayai na kuku ziliwahi kuagizwa kutoka nje.

Kwa mujibu wa Serikali ya Tanzania, utekelezaji wa kanuni hizo unalenga kuongeza ajira, kukuza nafasi za uongozi kwa wazawa na kuimarisha mchango wa sekta ya madini katika uchumi wa taifa.

Katika miaka ya hivi karibuni, Tanzania imechukua hatua kadhaa za kuimarisha sekta hiyo, ikiwemo ujenzi wa viwanda vya kuchakata madini, maabara, pamoja na marekebisho ya baadhi ya sheria zilizokuwa zikionekana kuwa kandamizi kwa wazawa.

Hata hivyo, Serikali inakiri kuwa changamoto kubwa imekuwa kwenye utekelezaji wa sheria hizo.

Wizara ya Madini sasa imetunga kanuni mpya zinazoweka zuio kwa zaidi ya bidhaa 20 kufanywa na wageni, hatua inayolenga kuhakikisha Watanzania wanapata manufaa halisi ya rasilimali za madini zilizopo nchini.

Soma zaidi
Jeshi la Benin lawaua 'magaidi' 45 kaskazini mwa nchi
Nchi za Afrika zaunga mkono Venezuela baada ya operesheni ya kijeshi ya Marekani iliyomlenga Maduro
Somalia yashtumu ziara ya waziri wa mambo ya nje wa Israel Somaliland, ikiitaja kama ‘uvamizi’
Mahakama ya Tunisia yawaachilia huru wafanyakazi wa NGO waliokamatwa kwa kuwasaidia wahamiaji
Baraza la Makanisa nchini Kenya lajitenga na mhubiri anayedai miujiza 'Nabii Owour'
Misri imepokea watalii milioni 19 mwaka 2025: Waziri
Rais Touadera achaguliwa tena kuwa rais wa Jamhuri ya Afrika ya Kati
Washukiwa wa ugaidi washambulia mgodi wa dhahabu, wawateka wafanyakazi nchini Mali
Vita vya Sahel na changamoto za makundi ya kigaidi
Mahakama Kuu ya Guinea yamthibitisha Doumbouya mshindi wa uchaguzi
Jeshi la Sudan lazuia shambulio la droni la RSF kwenye bwawa kuu na maeneo ya kijeshi
Rais William Ruto apendekeza adhabu ya kifo kwa wauzaji wa dawa za kulevya
Nigeria yaagiza msako mkali baada ya watu wenye silaha kufanya mauaji katika jimbo la Niger
Tanzania yaaga mashindano ya AFCON 2025
Radi yaua watu wawili na kuwajeruhi wengine 150 nchini Afrika Kusini
AU inaeleza 'wasiwasi mkubwa', Afrika Kusini inaomba mkutano wa dharura wa UN juu ya Venezuela
Madaktari wa Sudan wanaonya kuhusu tishio la janga la kibinadamu kusini mwa Kordofan
Kenya yaomboleza ndovu maarufu 'super tusker' Craig, aliyefariki akiwa na umri wa miaka 54
Zambia kuwa mwenyeji wa mkutano wa mawaziri wa ulinzi kuhusu mzozo wa DR Congo
Mapigano mapya yamezuka kati ya vikosi vya DRC na waasi wa M23 karibu na mji muhimu wa Uvira