| Swahili
AFRIKA
2 DK KUSOMA
Ndege iliyokuwa imembeba makamu wa rais wa Malawi Chilima haionekani
Ndege ya Jeshi la Ulinzi la Malawi "haikuonekana tena kwenye rada" baada ya kuondoka katika mji mkuu, Lilongwe, Jumatatu asubuhi
Ndege iliyokuwa imembeba makamu wa rais wa Malawi Chilima haionekani
#DLZ18 : Mahojiano na Makamu wa Rais Saulos Chilima, ambaye amesimama kama mgombeaji wa upinzani katika uchaguzi wa Mei / Picha: AFP / AFP
10 Juni 2024

Ndege ya kijeshi iliyokuwa imembeba Makamu wa Rais wa Malawi, Saulos Chilima, imeripotiwa kupotea baada ya kushindwa kutua Jumatatu asubuhi, serikali ilisema.

"Juhudi zote za mamlaka za anga kuwasiliana na ndege hiyo tangu ilipopotea kwenye rada zimegonga mwamba hadi sasa," serikali ilisema katika taarifa.

Chilima, mwenye umri wa miaka 51, alikuwa ndani ya ndege ya Jeshi la Ulinzi la Malawi iliyotoka mji mkuu wa Lilongwe saa 3:17 asubuhi (0717 GMT), ikiongeza kuwa operesheni za utafutaji na uokoaji zinaendelea.

Ndege ya Jeshi la Ulinzi la Malawi "ilipotea kwenye rada" baada ya kuondoka mji mkuu, Lilongwe, Jumatatu asubuhi.

Ndege hiyo ilipangwa kutua katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mzuzu saa 4:02 asubuhi, kulingana na taarifa hiyo.

Rais aliagiza operesheni ya utafutaji na uokoaji baada ya maafisa wa anga kushindwa kuwasiliana na ndege hiyo.

pata habari zaidi kupitia whatsapp channels

CHANZO:AFP