| Swahili
AFRIKA
2 DK KUSOMA
Vifo kutokana na maporomoko ya udongo Uganda vimefikia 13
Eneo la kutupia taka, linalojulikana kama Kiteezi, limetumika kama dampo pekee la takataka la Kampala kwa miongo kadhaa na limegeuka kuwa kilima kikubwa.
Vifo kutokana na maporomoko ya udongo Uganda vimefikia 13
Wakaazi wamelalamikia kwa muda mrefu taka hatari zinazochafua mazingira na kuwa hatari kwa wakaazi./ Picha : Reuters  / Others
11 Agosti 2024

Idadi ya vifo kutokana na maporomoko ya udongo katika eneo kubwa la kutupa taka katika mji mkuu wa Uganda Kampala imeongezeka hadi 13, polisi walisema Jumapili, huku waokoaji wakiendelea kuwatafutra manusura.

Baada ya mvua kubwa katika wiki za hivi majuzi, sehemu ya taka kutoka eneo pekee la dampo la jiji ilisambaratika siku ya Ijumaa, na kuzikandamiza na kuzika nyumba kwenye ukingo wa tovuti hiyo huku wakazi wakilala.

Siku ya Jumamosi, Mamlaka ya Jiji la Kampala iliweka idadi ya waliofariki kuwa wanane.

"Tunao hivi punde zaidi ni watu 13 waliofariki, lakini huduma za uokoaji zinaendelea," alisema msemaji wa polisi Patrick Onyango.

Takriban watu 14 wameokolewa hadi sasa, alisema, akiongeza kuwa wengine bado wamenaswa lakini idadi hiyo haijulikani.

Mahema yamejengwa kuwahifadhi wale waliohamishwa na maporomoko ya ardhi, Msalaba Mwekundu wa Uganda ulisema.

Eneo la kutupia taka, linalojulikana kama Kiteezi, limetumika kama dampo pekee la takataka la Kampala kwa miongo kadhaa na limegeuka kuwa kilima kikubwa.

Wakaazi wamelalamikia kwa muda mrefu taka hatari zinazochafua mazingira na kuwa hatari kwa wakaazi.

Pata habari zaidi kupitia Whatsapp channels

CHANZO:Reuters