Raia wa Afrika Kusini siku ya Alhamisi waliandamana nje ya Ubalozi wa Marekani mjini Pretoria, wakishtumu mashambulizi ya hivi majuzi ya kijeshi nchini Venezuela na kutekwa kwa Rais Nicolas Maduro na mkewe Cilia Flores.
“Tuko hapa kutuma ujumbe wa wazi kuwa namna Marekani inavyojifanya na tabia hii ya kijambazi haikubaliki na kwamba Afrika Kusini haitokubali hilo,” Muhammed Desai wa Shirikisho la Marekani na Latino la Afrika Kusini ameiambia Anadolu.
Desai anasema anaunga mkono msimamo wa serikali ya Afrika Kusini katika kushtumu mashambulizi ya Marekani nchini Venezuela. “Tunatoa wito wa kuachiliwa mara moja kwa Rais Nicholas Maduro,” alisema.
Maandamano hayo yaliyoandaliwa na vyama vya wafanyakazi vya Afrika Kusini, vyama vya kisiasa, vyama vya wanafunzi na mashirika yasiyokuwa ya kiserikali yaliungwa mkono na watu wengi waliokusanyika nje ya ubalozi wa Marekani.
Solly Mapaila, katibu mkuu wa Chama cha Kikomunisti cha Afrika Kusini (SACP),alishtumu kile alichokisema uingiliaji wa masuala ya ndani ya nchi ya Venezuela kwa Marekani na kutaka Maduro na mkewe waachiliwe bila masharti yoyote.
“Muachilie huru Rais Nicholas Maduro, Muachilie huru Cilia Flores, hatutaki ukoloni, maisha marefu kwa Venezuela,” alisikika akiwa pamoja na waandamanaji waliokuwa wamevaa fulana nyekundu.















