| Swahili
AFRIKA
1 dk kusoma
Umoja wa Afrika watoa wito wa 'kupunguzwa uhasama' baada ya Marekani na Israel kushambulia Iran
Mwenyekiti wa Tume ya Umoja wa Afrika (AUC), Mahamoud Ali Youssouf, anatoa wito "kujizuia, kupunguzwa uhasama na kurejelewa mazungumzo endelevu".
Umoja wa Afrika watoa wito wa 'kupunguzwa uhasama' baada ya Marekani na Israel kushambulia Iran
Moshi unapanda angani baada ya mlipuko huko Tehran, Iran, Jumamosi, Februari 28, 2026. / AP / AP
28 Februari 2026


Umoja wa Afrika ulihimiza viongozi wenye busara kuonyesha utulivu na subira siku ya Jumamosi baada ya Marekani na Israel kufanya mashambulizi dhidi ya Iran, na kuonya kwamba migogoro inaweza kuhatarisha zaidi maisha ya watu katika kanda hilo.

Mkuu wa shirika hilo barani Afrika, Mahamoud Ali Youssouf alitoa wito wa "kujizuia, na kurejelewa mazungumzo endelevu".

"Kuongezeka uhasama zaidi kunahatarisha kudorora kwa usalama na utulivu duniani, kukiwa na athari kubwa kwa masoko ya nishati, usalama wa chakula, na ustahimilivu wa kiuchumi -- hasa katika Afrika, ambako migogoro na shinikizo la kiuchumi bado ni kubwa."

Mashambulizi hayo yanakuja huku kukiwa na mvutano unaoongezeka kuhusu mpango wa nyuklia wa Iran ilihali mazungumzo yanafanyika na Marekani.

Mashahidi waliripoti mlipuko mkubwa katika mji mkuu wa Iran, Tehran, na moshi mkubwa ukipanda, wakati serikali ya Irani bado haijatoa maoni, shirika la habari la Reuters linaripoti.

Milipuko pia ilisikika huko Isfahan, Qom, Karaj na Kermanshah, kulingana na Shirika la Habari la Fars.

CHANZO:TRT Afrika