| Swahili
AFRIKA
1 dk kusoma
Benin yawakamata watu karibu 30 kuhusiana na jaribio la mapinduzi
Benin imewakamata watu takriban 30, wengi wao wanajeshi, kwa madai ya kuhusika na jaribio la mapinduzi lililotibuliwa mwezi huu, vyanzo vya kisheria vimeiambia AFP.
Benin yawakamata watu karibu 30 kuhusiana na jaribio la mapinduzi
Jaribio la mapinduzi lilitibuliwa nchini Benin Disemba 7, 2025. / Reuters
tokea masaa 9

Benin imewakamata watu karibu 30, wengi wao wakiwa wanajeshi, kwa madai ya kuhusika na jaribio la mapinduzi lililotibuliwa mwezi huu, vyanzo vya kisheria vimeiambia AFP.

Wanajeshi walijitokeza kwenye televisheni ya taifa Disemba 7 kutangaza kuwa Rais Patrice Talon amepinduliwa lakini jaribio hilo la mapinduzi lilitibuliwa na wanajeshi watiifu.

Watu kadhaa waliuawa na kiongozi wa yaliyodaiwa kuwa mapinduzi, Luteni Kanali Pascal Tigri, na wanajeshi walioasi hawajulikani waliko.

Siku ya Jumatatu, watu karibu 30 wanaoshtumiwa walifikishwa mbele ya mwendesha mashtaka maalum wa mahakama ya uhalifu wa kiuchumi na ugaidi katika mji wa Cotonou, vyanzo vilisema siku ya Jumanne.

Kukamatwa kabla ya kesi

Walizuiwa kabla ya kesi siku ya pili baada ya shauri lao kusikilizwa, waliongeza.

Wanashtakiwa na "uhaini", "mauaji" na "kuhatarisha usalama wa nchi", vyanzo hivyo vilisema.

Kulikuwa na ulinzi mkali katika maeneo ya mahakamani, mwandishi wa habari wa AFP alishuhudia.

Kwingineko, Chabi Yayi, mtoto wa kiume wa rais wa zamani wa Benin na mwanasiasa wa upinzani sasa hivi Thomas Boni Yayi, aliachiliwa huru siku ya Jumatatu baada ya kuhojiwa siku ya Jumatatu.

CHANZO:TRT Afrika