Benin imewakamata watu karibu 30, wengi wao wakiwa wanajeshi, kwa madai ya kuhusika na jaribio la mapinduzi lililotibuliwa mwezi huu, vyanzo vya kisheria vimeiambia AFP.
Wanajeshi walijitokeza kwenye televisheni ya taifa Disemba 7 kutangaza kuwa Rais Patrice Talon amepinduliwa lakini jaribio hilo la mapinduzi lilitibuliwa na wanajeshi watiifu.
Watu kadhaa waliuawa na kiongozi wa yaliyodaiwa kuwa mapinduzi, Luteni Kanali Pascal Tigri, na wanajeshi walioasi hawajulikani waliko.
Siku ya Jumatatu, watu karibu 30 wanaoshtumiwa walifikishwa mbele ya mwendesha mashtaka maalum wa mahakama ya uhalifu wa kiuchumi na ugaidi katika mji wa Cotonou, vyanzo vilisema siku ya Jumanne.
Kukamatwa kabla ya kesi
Walizuiwa kabla ya kesi siku ya pili baada ya shauri lao kusikilizwa, waliongeza.
Wanashtakiwa na "uhaini", "mauaji" na "kuhatarisha usalama wa nchi", vyanzo hivyo vilisema.
Kulikuwa na ulinzi mkali katika maeneo ya mahakamani, mwandishi wa habari wa AFP alishuhudia.
Kwingineko, Chabi Yayi, mtoto wa kiume wa rais wa zamani wa Benin na mwanasiasa wa upinzani sasa hivi Thomas Boni Yayi, aliachiliwa huru siku ya Jumatatu baada ya kuhojiwa siku ya Jumatatu.





















