| Swahili
UTURUKI
2 dk kusoma
Waziri wa Mambo ya Nje wa Uturuki ashiriki mazungumzo ya awamu ya pili ya mpango wa amani wa Gaza
Mazungumzo hayo yalifuatia mikutano ya awali iliyofanyika Miami, Florida, nchini Marekani mwishoni mwa Disemba 2025.
Waziri wa Mambo ya Nje wa Uturuki ashiriki mazungumzo ya awamu ya pili ya mpango wa amani wa Gaza
Mkutano huo uliwaleta pamoja maafisa kutoka Marekani, Misri na Qatar kujadili maandalizi ya hatua inayofuata ya mpango wa amani wa Gaza. / / AA
12 Januari 2026

Waziri wa Mambo ya Nje wa Uturuki, Hakan Fidan, ameshiriki katika mkutano uliofanyika kupitia mtandaoni kilichojadili maandalizi ya awamu ya pili ya mpango wa amani wa Gaza.

Kwa mujibu wa vyanzo vya wizara ya mambo ya nje ya Uturuki, Fidan alijiunga na mkutano huo wa mtandaoni siku ya Jumatatu kama mwendelezo wa mazungumzo yaliyofanyika Miami, Florida, nchini Marekani mwishoni mwa Disemba 2025.

Mkutano huo uliwakutanisha maafisa kutoka Marekani, Misri na Qatar ili kujadili maandalizi ya hatua inayofuata ya mpango wa amani wa Gaza.

Makubaliano ya kusitisha mapigano yalianza kutekelezwa Gaza tarehe 10 Oktoba chini ya mpango wa vipengele 20 wa Rais wa Marekani Donald Trump, hatua iliyosimamisha mashambulizi ya Israel yaliyodumu kwa miaka miwili, ambayo yamesababisha vifo vya zaidi ya watu 70,000—hasa wanawake na watoto—na kujeruhi karibu watu 171,000 tangu Oktoba 2023.

Diplomasia

Kwa mujibu wa vyanzo vya kidiplomasia vya Uturuki, Fidan pia alifanya mazungumzo ya simu kwa nyakati tofauti na mawaziri wa mambo ya nje wa Ugiriki na Uzbekistan.

Fidan na Waziri wa Mambo ya Nje wa Ugiriki, Giorgos Gerapetritis, walijadili uhusiano wa mataifa mawili pamoja na maendeleo ya kikanda.

Katika mazungumzo mengine ya simu, Fidan alizungumza na Waziri wa Mambo ya Nje wa Uzbekistan, Bakhtiyor Saidov. Wawili hao walijadili uhusiano wa mataifa mawili pamoja na masuala ya kikanda.

Pia walizungumzia maandalizi ya mkutano ujao wa Baraza la Ushirikiano wa Kimkakati wa ngazi ya juu kati ya nchi hizo mbili.

Hakuna maelezo ya ziada kuhusu mazungumzo hayo yaliyotolewa.

CHANZO:AA
Soma zaidi
Rais wa Uturuki awasili Ethiopia kwa ziara rasmi
Emine Erdogan awatuza wasukuma mabadiliko wakati wa makala ya 7 ya tuzo za TRT World
Rais wa Uturuki aelekea Ethiopia kwa ziara ya kikazi
Waziri Mkuu wa Somalia apongeza uchimbaji mafuta wa 'kihistoria' baharini na Uturuki
Uturuki inapanua utaalam wa reli, kutoa mafunzo kwa wafanyakazi Afrika, Asia
Erdogan: Uturuki inaendelea kutafuta amani ya kanda licha hofu iliyopo ulimwenguni
Rais wa Uturuki ateuwa Waziri mpya wa Katiba na Mambo ya Ndani katika mabadiliko ya Baraza la Mawazi
Fidan wa Uturuki akataa mashambulizi ya anga kama njia ya kubadilisha uongozi wa Iran
Makamu wa Rais wa Uturuki akutana na balozi wa Brazil
Idadi ya watu nchini Uturuki yafikia milioni 86 kwa mwaka 2025
Uturuki yalaani shambulizi la RSF nchini Sudan
Matetemeko ya ardhi ya Uturuki 2023 yalisababisha hasara ya dola bilioni 250: Erdogan
Fidan wa Uturuki akutana na Kamishna wa Maswala ya Wanachama wa EU, kujadili masuala ya ushirikiano
Rais wa Uturuki aadhimisha kumbukumbu ya miaka 3 ya tetemeko la ardhi
Uturuki imelaani shambulizi la kigaidi nchini Nigeria lililoua takriban watu 170
Uturuki kuimarisha uwepo wake wa kijeshi kuisaidia Somalia kupambana na ugaidi
Uturuki na Saudi Arabia kuimarisha ushirikiano wa ulinzi na uwekezaji katika ndege za kivita za KAAN
Mke wa Rais wa Uturuki amekutana na mwenzake wa Misri jijini Cairo
Erdogan na Sisi waimarisha ushirikiano kati ya Uturuki na Misri wajadili Gaza na migogoro ya kikanda
Kikao cha mwisho cha Jukwaa la Biashara kati ya Uturuki na Misri chafunguliwa jijini Cairo