| Swahili
AFRIKA
1 dk kusoma
Zaidi ya wahamiaji 40 wafariki katika ajali ya boti pwani ya Libya
IOM inataka kuongezeka kwa ushirikiano wa kimataifa na hatua za ulinzi thabiti, ikijumuisha upanuzi wa njia salama na za kisheria za uhamiaji, ili kupunguza vifo.
Zaidi ya wahamiaji 40 wafariki katika ajali ya boti pwani ya Libya
IOM inataka jitihada zaidi kufanyika ili kuzuia majanga ya vifo vya wahamiaji katika bahari ya Mediterenia. / Others
tokea masaa 12

Takriban wahamiaji 53, ikiwa ni pamoja na watoto wawili wachanga, wamekufa au hawajulikani walipo baada ya boti iliyokuwa imebeba watu 55 kuzama karibu na pwani ya Libya, taarifa hiyo ya Jumatatu ni kwa mujibu wa Shirika la Kimataifa la Uhamiaji (IOM).

Boti hiyo ilipinduka kaskazini mwa mji wa pwani wa Zuwara Februari 6, na wanawake wawili tu raia wa Nigeria waliokolewa na mamlaka za Libya.

Kwa mujibu wa waliookolewa, mwanamke mmoja alimpoteza mume wake katika ajali hiyo, wakati mwenzake alipoteza watoto wawili wachanga baada ya boti iliyojaa kupita kiasi kuanza kupenyeza maji na kuzama takriban baada ya saa sita za safari.

IOM ilisema wahamiaji na wakimbizi hao, wote wakiwa na utaifa wa Kiafrika, walitoka Al-Zawiya mwendo wa usiku Februari 5, wakijaribu kuvuka Bahari ya Mediterania kuelekea Ulaya. IOM ilithibitisha kutoa msaada wa haraka kwa waliookolewa ikiwemo kuwapa matibabu.

Janga hili linaongeza idadi ya matukio ya kifo vinayoongezeka kwa wahamiaji haramu kupitia Bahari ya Mediterania.