| Swahili
AFRIKA
1 dk kusoma
Jeshi la Benin lawaua 'magaidi' 45 kaskazini mwa nchi
Siku ya Jumanne jeshi la Benin limesema limewaua "magaidi" 45 katika kipindi cha miezi mitatu ya operesheni dhidi ya ugaidi kaskazini mwa Benin.
Jeshi la Benin lawaua 'magaidi' 45 kaskazini mwa nchi
Kati ya Oktoba na Disemba 2025, wanajeshi wa Benin "waliwakata makali" magaidi 45 na kuwakamata washukiwa 7. / Reuters
6 Januari 2026

Siku ya Jumanne jeshi la Benin limesema limewaua magaidi 45 katika kipindi cha miezi mitatu ya operesheni dhidi ya ugaidi kaskazini mwa Benin.

Makundi yenye uhusiano na magaidi wa Al Qaeda huwa yanatishia usalama kaskazini mwa nchi.

2022, Benin ilipeleka takriban wanajeshi 3,000 kwa operesheni yake ya "Mirador" dhidi ya magaidi, na kwa sasa wameajiri wanajeshi wengine 5,000 kuimarisha usalama eneo la kaskazini.

Kati ya Oktoba na Disemba 2025, jeshi hilo "liliwakata makali magaidi 45 na kuwakamata washukiwa 7, ambao walifikishwa kwa mamlaka za mahakama", ulisema ujumbe wa jeshi ulioonekana na AFP.

'Kuwa makini bado ni muhimu'

Silaha, pikipiki, madumu ya petroli na magwanda ya jeshi yalipatikana "wakati wa makabiliano na adui ‘‘, Jeshi la Benin (FAB) lilisema, likipongeza "kuimarika" kwa uwezo wake.

"Shinikizo linalowekwa na FAB sasa linafanya iwe vigumu kwa makundi yenye silaha kuwepo kwa muda mrefu katika maeneo ya mpaka," jeshi lilisema.

Lakini liliongeza kwamba "kuwa makini bado ni muhimu."

CHANZO:TRT Afrika Swahili
Soma zaidi
Umoja wa Afrika waitaka Israel kubatilisha utambuzi wa Somaliland
Nchi za Afrika zaunga mkono Venezuela baada ya operesheni ya kijeshi ya Marekani iliyomlenga Maduro
Somalia yashtumu ziara ya waziri wa mambo ya nje wa Israel Somaliland, ikiitaja kama ‘uvamizi’
Mahakama ya Tunisia yawaachilia huru wafanyakazi wa NGO waliokamatwa kwa kuwasaidia wahamiaji
Baraza la Makanisa nchini Kenya lajitenga na mhubiri anayedai miujiza 'Nabii Owour'
Misri imepokea watalii milioni 19 mwaka 2025: Waziri
Rais Touadera achaguliwa tena kuwa rais wa Jamhuri ya Afrika ya Kati
Washukiwa wa ugaidi washambulia mgodi wa dhahabu, wawateka wafanyakazi nchini Mali
Vita vya Sahel na changamoto za makundi ya kigaidi
Tanzania yapiga marufuku wageni kutoa baadhi ya huduma katika sekta ya madini, kulinda wazawa
Mahakama Kuu ya Guinea yamthibitisha Doumbouya mshindi wa uchaguzi
Jeshi la Sudan lazuia shambulio la droni la RSF kwenye bwawa kuu na maeneo ya kijeshi
Rais William Ruto apendekeza adhabu ya kifo kwa wauzaji wa dawa za kulevya
Nigeria yaagiza msako mkali baada ya watu wenye silaha kufanya mauaji katika jimbo la Niger
Tanzania yaaga mashindano ya AFCON 2025
Radi yaua watu wawili na kuwajeruhi wengine 150 nchini Afrika Kusini
AU inaeleza 'wasiwasi mkubwa', Afrika Kusini inaomba mkutano wa dharura wa UN juu ya Venezuela
Madaktari wa Sudan wanaonya kuhusu tishio la janga la kibinadamu kusini mwa Kordofan
Kenya yaomboleza ndovu maarufu 'super tusker' Craig, aliyefariki akiwa na umri wa miaka 54
Zambia kuwa mwenyeji wa mkutano wa mawaziri wa ulinzi kuhusu mzozo wa DR Congo