Misaada yapungua Sudan Kusini huku waliopoteza makazi wakikabiliana na majanga
AFRIKA
2 dk kusoma
Misaada yapungua Sudan Kusini huku waliopoteza makazi wakikabiliana na majangaWamejikuta katikati ya mzozo na athari za tabianchi, jamii za waliopoteza makazi yao Sudan Kusini zinajikuta zikikabiliana na vurugu, mafuriko na kukosa misaada ya kutosha
Kufurika kwa mito katika wiki za hivi karibuni, kumesababisha watu zaidi 100,000 kuondoka katika makazi yao. Picha: UNHCR/Tiksa Negeri / Wengine
14 Oktoba 2025

Adhieu Marial amesimama kwa kile kilichobaki kwa nyumba yake katika Jimbo la Unity la Sudan Kusini, akitathmini kilichobaki baada ya mafuriko.

"Kwanza, tumekimbia mashambulizi ya risasi. Sasa,tunakimbia maji," mama huyo mwenye watoto wanne ameiambia TRT Afrika.

Katika wiki za hivi karibuni, mito iliyofurika imefunika sehemu kubwa ya majimbo ya Jonglei, Upper Nile na Unity, na kusababisha watu zaidi ya 100,000 kuachwa bila makazi yao. Wengi wao walikuwa ndiyo wanaanza tu kujenga upya maisha yao baada ya kulazimika kukimbia mapigano yaliyotibuka mapema mwaka huu.

Sasa, mafuriko yana watatiza tena.

Adhieu, ni miongoni mwa wale wanaojaribu kuweka sawa maisha yao huku wakikabiliana na janga lingine, ameamua kuangazia mustakabali wake.

"Mafuriko yalifunika nyumba yetu, lakini bado tuna matumaini. Kwa mabati haya tuliyopata kutoka kwa mashirika ya misaada, angalau tumepata sehemu ya kujistiri. Watoto wangu wako salama kwa sasa," anasema Adhieu, akiwa anawakilisha hisia za maelfu ya watu.

Matatizo mbalimbali

Kila siku, kuna matumaini kwa wale waliopoteza makazi yao Sudan Kusini.

Shirika linaloshughulikia wakimbizi la Umoja wa Mataifa (UNHCR) limeonya kuwa kama mafuriko yataendelea, watu hadi ya 400,000 watakuwa wamepoteza makazi yao kufikia mwisho wa mwaka.

"Tunakabiliwa na matatizo ya mabadiliko ya tabianchi na migogoro, ambapo tatizo moja linasababisha tatizo lingine," Eunice Njeri, mratibu anayefanya kazi na mashirika mbalimbali yasiyokuwa ya kiserikalli Sudan Kusini, ameiambia TRT Afrika.

"Familia moja iliyopoteza makazi yake kutokana na vita inafika katika eneo lingine, na wanapata mkosi wa kuondoka pia kwenye sehemu hiyo kutokana na mafuriko.Kuhamahama huku kunafanya iwe vigumu kusaidia familia na kufanya hali kuwa ngumu zaidi kwa watu."

Suluhu, Njeri anasema, iko katika kuweka mikakati ya pamoja ya kukabiliana na matatizo badala ya kuyaangalia kama matatizo tofauti. "Misaada kutoka kwa jamii ya kimataifa yanatakiwa kuwa mahsusi kwa ajili ya migogoro wanayopitia watu hawa," anasema.

Elimu

Huku kukiwa na changamoto, kuna matumaini katika suala la elimu.

Walimu wana matumaini ya kuendeleza elimu hata wakati shule na madarasa yakigeuka kuwa vidimbwi.

"Hii ni changamoto kubwa," anasema Puot Kuol, mwalimu huko Upper Nile. "Lakini hatuwezi kukata tamaa. Vita vimetatiza elimu, na sasa mafuriko yamesababisha changamoto nyingine. Lakini sasa tunatafuta suluhu – kufunza chini ya miti, ndani ya hema lilitolewa la msaada, popote tunapoweza. Watoto hawa ni mustakabali wa Sudan Kusini. Tutapata njia ya kuwafunza."

CHANZO:TRT Afrika
Soma zaidi
Rais Salva Kiir wa Sudan Kusini amfuta kazi makamu wake
Duma wa Botswana aipa India zawadi ya duma 8
Kesi ya Roger Lumbala wa DRC yaanza kusikilizwa
Kesi za ubakaji, watoto kupotea zaripotiwa Darfur, Sudan – Umoja wa Mataifa
Ugonjwa wa Kichaa cha mbwa barani Afrika: Janga linaloendelea kuathiri maisha japo linaepukika
Libya yatakiwa kufunga vituo vya kuwazuilia wahamiaji katika mkutano wa Umoja wa Mataifa
Rais Museveni aonya kuzuka kwa vita endapo nchi za Afrika zitashindwa kufikia Bahari ya Hindi
UN: Milioni 11 wanawake na wasichana wanabeba uzito mkubwa wakati njaa ya Sudan inaendelea kupamba moto
Ethiopia yachagguliwa kuwa mwenyeji wa mkutano wa Umoja wa Mataifa kuhusu hali ya hewa, COP32
Ghana yafichua sababu ya ajali ya helikopta iliyoua watu wanane, wakiwemo mawaziri, mwezi Agosti
Nigeria yaanzisha uchunguzi baada ya kukamata kilo 1,000 za kokeini yenye thamani ya $235M
Kenya kuanzisha balozi zake mpya Vatican City, Denmark na Vietnam
Mtoto wa Gaddafi aachiliwa huru baada ya miaka kumi gerezani
Kuanzia vifo vya taratibu hadi mauaji ya ukatili: Kutoweka kwa utu Al Fasher
Zaidi ya mataifa 20 yanalaani ukatili wa RSF nchini Sudan, na kutaka kukomeshwa kwa ghasia
Rais wa Misri, afisa mkuu wa usalama wa Urusi kujadili ushirikiano wa kijeshi
Maelfu ya wananchi wanashikiliwa katika hali mbaya sana katika Al Fasher, Sudan: madaktari
Makamu wa Rais wa Marekani JD Vance aghairi ziara iliyopangwa nchini Kenya
‘Mauaji ya waandamanaji ni chukizo mbele za Mungu’
Jeshi la Sudan lazima shambulio la RSF katika mji wa Babnousa huko Kordofan Magharibi