Bassirou Diomaye Faye: Rais wa Senegal
Rais wa Senegal Bassirou Diomaye Faye.
Bassirou Diomaye Faye: Rais wa Senegal
Basirou Diomaye Faye ni rais wa taifa la Senegal lililoko Afrika Magharibi. Taifa hilo lina watu takriban watu milioni 19.
tokea siku moja

Jina kamili la kiongozi wa taifa hilo ni Basirou Diomaye Diakhar Faye mzaliwa wa Ndiaganiao katika mji wa M’bour miaka 45 iliopita.

Ukiskia majina yanaumba maana yake ni hii kwa lugha ya Serer inayozungumzwa na baadhi ya watu wa Senegal na Gambia, jina ‘’Diomaye’’ maana yake ‘’Mheshimiwa’’ sasa limetimia au vipi?

Amekuwa rais wa nchi hiyo tangu mwaka April 2024. Yeye na Waziri Mkuu wake Ousmane Sonko walikutana wakiwa maafisa forodha.

Mwaka 2014 urafiki wao ukaimarika zaidi, Sonko alipounda chama cha kisiasa cha PASTEF.

Diomaye Faye alimsaidia sana Sonko katika uchaguzi wa urais wa 2019, lakini Sonko alimaliza wa tatu na asilimia 16 ya kura.

Kufa kufaana, mwaka 2021 Faye akawa Katibu Mkuu wa chama cha PASTEF baada ya Sonko kukamatwa.

Mwaka 2022 alijaribu kuunganisha upinzani na kufanikiwa kushinda viti 56 katika bunge la wajumbe 165. Alijaribu kutafuta umeya wa eneo la Ndianganao, lakini hakufanikiwa.

Alikamatwa mwaka 2023 kwa madai kadhaa kusambaza taarifa taarifa za uwongo ikiwa sehemu ya madai mengi aliyoshtumiwa nayo.

Kutokana na wasiwasi kuhusu mgombea wa urais wa chama cha PASTEF kwa kuwa Ousmane Sonko alikuwa yuko gerezani, chama hicho kilimchagua Faye licha ya yeye pia kuwa kizuizini.

Kwa kuwa chama cha PASTEF kilikuwa kimepigwa marufuku alikuwa agombee kama mgombea huru.

Aliachiliwa mwezi Machi, kabla ya hapo Sonko alitangaza kumuunga mkono. Kauli mbiu yake wakati wa kampeni  za uchaguzi wa 2024 kwa lugha ya Wolof ilikuwa ‘’Diomaye mooy Sonko’’ maana yake ‘’Diomaye ni Sonko’’ kusisitiza ukaribu wao.

Alishinda uchagui huo wa mwezi Machi kwa asilimia 54 na kumfanya kuwa mgombea wa kwanza kushinda karika duru ya kwanza tangu nchi hiyo ya Senegal ilipopata uhuru wake kutoka kwa Ufaransa 1960.

Aliapishwa rasmi tarehe 2 Aprili kuwa rais na hatua ya kwanza aliyochukuwa ni kumteua Ousmane Sonko Waziri Mkuu ambaye aliwasilisha baraza lake la mawaziri siku tatu baadaye.

Rais Diomaye Faye ana wake wawili na amempa mtoto wake mmoja jina la rafiki yake Ousmane Sonko kwa heshima ya ukaribu wao.  

CHANZO:TRT Afrika Swahili
Soma zaidi
Rais wa Nigeria athibitisha kuuawa kwa jenerali wa jeshi
Wataalamu wa Afrika watoa wito wa kukaguliwa tathmini ya viwango vya mikopo kwa bara
Eswatini yapokea dola milioni 5.1 kupokea wahamiaji waliofurushwa Marekani, waziri anasema
Gabon yatia saini makubaliano ya kihistoria ya ufadhili wa hali ya hewa kwa misitu ya mvua ya Congo
Wanajeshi wa RSF wameripotiwa kupata hasara kubwa katika jimbo la Kordofan Kaskazini nchini Sudan
CAF yatangaza wasimamizi maarufu wa sherehe ya Tuzo za CAF 2025
Jeshi la Somalia limewauwa magaidi 11 wa Al Shabab na kuzuia shambulio la kujitoa muhanga
Tanzania huenda ikakabiliwa na changamoto kupata mikopo kutoka nje, amesema Rais Samia
Sura mpya Baraza la Mawaziri Tanzania
Cape Verde, Mauritius na Ushelisheli wafanikiwa kuangamiza surua na  rubela
Rais wa Sudan Kusini Kiir amrejesha makamu wa rais katika mabadiliko ya baraza la mawaziri
Zaidi ya watu 100,000 wamekimbia makazi yao kutoka Al Fasher ya Sudan tangu kutwaliwa na RSF
Rais wa Tanzania amteua binti na mkwe wake katika Baraza la Mawaziri
Rais Samia amteua waziri mpya wa fedha, awaacha mawaziri wa mambo ya nje na madini madarakani
Tovuti za taasisi za serikali ya Kenya zashambuliwa
Mgodi waporomoka DRC na kuua watu wasiopungua 32
Wahamiaji 4 wafariki baada ya boti mbili zilizokuwa zimebeba makumi ya watu kuzama pwani ya Libya
Kikundi cha matabibu kinaripoti visa ya ubakaji wa wasichana wa Al Fasher baada ya RSF kuteka
Mlipuko wa virusi vya Marburg umethibitishwa kusini mwa Ethiopia
DR Congo, M23 wasaini makubaliano ya amani 'ya kihistoria' nchini Qatar