ULIMWENGU
2 dk kusoma
ICC yamshtaki Rais wa zamani wa Ufilipino Duterte kwa uhalifu dhidi ya binadamu
Rodrigo Duterte anadaiwa kuwa “mhusika asiye wa moja kwa moja” katika mauaji ya mamia ya watu.
ICC yamshtaki Rais wa zamani wa Ufilipino Duterte kwa uhalifu dhidi ya binadamu
Wakili wa Duterte anadai mteja wake anakumbwa na ugonjwa wa “kupoteza fahamu”./
23 Septemba 2025

Rais wa zamani wa Ufilipino, Rodrigo Duterte, ameshtakiwa kwa uhalifu dhidi ya binadamu na Mahakama ya Kimataifa ya Jinai (ICC), ambapo anadaiwa kushiriki katika mauaji ya watu karibia 76 wakati wa kampeni yake ya “vita dhidi ya madawa ya kulevya”.

Mashtaka dhidi ya mwanasiasa huyo mwenye umri wa miaka 80, ambaye amekuwa gerezani nchini Uholanzi tangu mwezi Machi, yamewekwa wazi kwenye waraka uliochapishwa na ICC Jumatatu.

Mashtaka hayo pia yanahusiha sehemu moja ya kampeni kali ya kupambana na madawa ya kulevya iliyoongozwa na Duterte alipokuwa rais, ambayo ilisababisha vifo vya maelfu ya watu waliodaiwa kuwa wauzaji na watumiaji wa madawa ya kulevya.

Kulingana na waraka ya mashtaka wa ICC na kusainiwa na msaidizi wa mashtaka wa mahakama hiyo, Mame Mandiaye Niang, wakili wa mashtaka anaona kuwa Duterte ni mhusika wa moja kwa moja katika mauaji yaliyotokea kati ya mwaka 2013 na 2018.

Kesi ya kwanza inahusiana na kipindi chake akiwa Meya wa Jiji la Davao, ambapo anadaiwa kuwa “mhusika asiye wa moja kwa moja” katika mauaji 19 kati ya 2013 na 2016.

Mashtaka ya pili na ya tatu yanahusu miaka yake akiwa rais. Aidha kesi ya pili inahusu mauaji ya walengwa 14 waliodaiwa kuwa na umuhimu mkubwa kati ya 2016 na 2017, huku kesi ya tatu ikihusu mauaji 43 yaliyofanywa wakati wa operesheni za ‘kuondoa’ dhidi ya wahalifu wa ngazi ya chini kati ya 2016 na 2018.

Kati ya mauaji hayo 76 yalitekelezwa na polisi kwa mujibu wa ICC.

Hata hivyo mahakama inapaswa kwanza kuamua kama rais huyo wa zamani yuko katika hali nzuri ya kisheria kuweza kushtakiwa, baada ya wakili wake, Nicholas Kaufman, kupendekeza kesi hiyo ichelweshwe kwa muda usiojulikana kutokana na hali mbaya ya afya ya Duterte.

Kaufman amesema Duterte anakumbwa na ugonjwa wa “kupoteza fahamu”.

Duterte alikamatwa jijini Manila, mji mkuu wa Ufilipino, tarehe 11 Machi, na haraka akapelekwa Uholanzi ambapo amekuwa gerezani chini ya ICC. Duterte anasisitiza kuwa kukamatwa kwake ni kinyume cha sheria.

Wafuasi wa Duterte nchini Ufilipino wanasema kuwa kukamatwa kwake ni siasa na ni matokeo ya mzozo kati ya familia yake na rais wa sasa wa Ufilipino, Ferdinand Marcos Jr.

CHANZO:Al Jazeera
Soma zaidi
Maseneta wa Marekani wanamtaka Trump kuchukua msimamo thabiti dhidi ya unyakuzi wa West Bank
Waziri Mkuu wa Israel amfuta kazi msaidizi wake mkuu wa usalama kwa mtafaruku juu ya Gaza
Mbu wapatikana nchini Iceland kwa mara ya kwanza
Kiongozi Mkuu wa Iran, Khamenei, apinga madai kuwa Marekani imeharibu uwezo wa nyuklia wa nchi yake
Mashambulizi mapya ya Israel yawauwa takriban Wapalestina 21 huko Gaza licha ya kusitishwa kwa vita
Gaza inaishutumu Israel kwa wizi wa viungo kutoka kwa Wapalestina, inataka uchunguzi wa kimataifa
ICC inakataa ombi la Israel la kukata rufaa kuhusu vibali vya kukamatwa kwa Netanyahu na Gallant
Israel yapunguza upatikanaji wa misaada kwa nusu, inazuia mafuta kuingia Gaza
Mabomu ambayo hayajalipuka yana hatari 'kubwa' huko Gaza, NGO yaonya
Marekani katika kizungumkuti cha kutumia dhahabu yake kulipia deni la taifa
'Sura mpya kwa amani' — Dunia inajibu baada ya kusaini hati rasmi ya kumaliza vita vya Gaza
Viongozi wa Marekani, Uturuki, Misri, na Qatar wamesaini makubaliano yanayositisha vita vya Gaza
Kuachiliwa kwa mateka kutaanza Gaza saa 11 alfajiri, vyombo vya habari vya Israel vinaripoti
Israel inadhulumu wafungwa Wapalestina kabla ya kuachiliwa chini ya makubaliano na Hamas, video inaonyesha
Trump, Sisi kushirikiana kuandaa mkutano wa Gaza huko Sharm el-Sheikh nchini Misri
Kiongozi wa upinzani wa Venezuela Maria Corina Machado ashinda Tuzo ya Amani ya Nobel ya 2025
Wapalestina 200,000 wanarejea kaskazini mwa Gaza huku wanajeshi wa Israel wakiondoka
Wanajeshi wa Marekani wawasili Israel kusaidia kufuatilia usitishaji mapigano Gaza
Trump ataungana na viongozi, wanadiplomasia kutoka Uturuki na wengine kwenye mkutano wa Gaza, Cairo
Kiongozi wa upinzani wa Venezuela Maria Corina Machado ashinda Tuzo ya Nobel ya Amani 2025