| Swahili
MICHEZO
1 dk kusoma
Kocha wa Zambia Moses Sichone hatoshelezi kanuni za CAF
Maafisa wa Zambia wanatarajia kutatua tatizo hilo kwa kubadilisha cheo cha kocha mkuu na kuwa kocha msaidizi anapokidhi masharti ya kustahiki nafasi hiyo.
Kocha wa Zambia Moses Sichone hatoshelezi kanuni za CAF
FILE: Moses Sichone aliteuliwa kuwa kocha mkuu wa Zambia mwezi uliopita. / Reuters / Reuters
20 Desemba 2025

Kocha mkuu wa Zambia Moses Sichone hawezi kukaa benchi kwani hana sifa zinazohitajika za Shirika la Soka Afrika (CAF), kwa mujibu wa ripoti.

Maafisa wa Chipolopolo (Copper Bullets) wanatarajia kutatua tatizo hilo kwa kumbadilishia cheo cha mchezaji huyo wa zamani wa kimataifa kuwa kocha msaidizi, kwani anakidhi vigezo vinavyotumika kwa nafasi hiyo.

Zambia wako Kundi A pamoja na Morocco, ambao wanachukuliwa kama wagombea wakuu wa taji, pamoja na Comoros na Mali.

Nigeria imetangaza kwamba kiungo anayekipiga mtanange nchini Uturuki, Wilfred Ndidi, atakuwa nahodha wa timu baada ya William Troost-Ekong, ambaye hivi karibuni alitangaza kustaafu kutoka kwenye mchezo wa kimataifa.

Nigeria watazindua kampeni yao ya Kundi C dhidi ya Tanzania huko Fes, kisha watazikabili Tunisia na Uganda katika mji huo huo.

CHANZO:Reuters