UTURUKI
2 dk kusoma
Uturuki imetuma “Meli ya Ukarimu” ya 17 yenye msaada wa tani 900 kuelekea Gaza
Uturuki imetuma “Meli ya Ukarimu” ya 17 ikiwa na tani 900 za misaada ya kibinadamu kuelekea Gaza, ikiwa ni sehemu ya juhudi endelevu za misaada baada ya kusitishwa kwa mapigano.
Uturuki imetuma “Meli ya Ukarimu” ya 17 yenye msaada wa tani 900 kuelekea Gaza
"Meli ya 17 ya Ukarimu," ya Uturuki iliyobeba msaada wa Gaza, imeondoka Bandari ya Mersin kuelekea Bandari ya Al Arish ya Misri Oktoba 14, 2025. /
14 Oktoba 2025

Meli hiyo, iliyopakiwa takribani tani 900 za chakula na mahitaji ya watoto wachanga, iliondoka Jumanne katika Bandari ya Kimataifa ya Mersin, kusini mwa Uturuki, kuelekea Bandari ya Al Arish nchini Misri.

Misaada hiyo imepangwa chini ya uratibu wa Idara ya Kudhibiti Majanga na Dharura ya Uturuki (AFAD) kwa ushirikiano na shirika la Hilali Nyekundu ya Misri, vile vile ilijumuisha misaada ya mashirika yasiyo ya kiserikali 17.

Mizigo hiyo ya msaada itapitia katika mpaka wa Karem Abu Salem kupitia Bandari ya Al Arish, bandari iliyo karibu zaidi na Ukanda wa Gaza.

Misaada hiyo, iliyotayarishwa kusaidia wakazi wa Gaza kukidhi mahitaji yao ya msingi, inajumuisha chakula tayari kuliwa, vyakula vya makopo na maziwa ya watoto wachanga.

Wakati wa hafla ya kuaga meli hiyo katika Bandari ya Mersin, Waziri wa Mambo ya Ndani wa Uturuki, Ali Yerlikaya, alisema: “Leo tunasema ‘Meli ya Ukarimu inaelekea Gaza.’ Chombo hiki cha Bahari ya Mediterania kimebeba tani 900 za chakula, vyakula vya makopo na maziwa ya watoto wachanga, na sasa kinaelekea Gaza.”

Tangu kuanza kwa mashambulizi ya mauaji ya halaiki ya Israel dhidi ya Gaza tarehe 7 Oktoba 2023, Uturuki imekuwa ikitoa misaada ya kibinadamu kupitia meli 16 na ndege 14 chini ya uratibu wa AFAD.

Wiki iliyopita, mkataba wa kusitisha mapigano ulifikiwa kama sehemu ya mpango wa Rais wa Marekani Donald Trump wa kumaliza kabisa vita vilivyowaua zaidi ya Wapalestina 67,000 na kuharibu eneo lote la Gaza.

CHANZO:AA