| Swahili
ULIMWENGU
2 dk kusoma
Israel imetuma masanduku yenye 'mafuvu ya vichwa na miili ya wanawake' ya Wapalestina huko Gaza
Aliyekuwa kiongozi wa chama cha Labour Jeremy Corbyn ameeleza ujumbe kutoka kwa mkurugenzi wa Hospitali ya Al-Shifa kuhusiana na kuwasilishwa kwa mabaki ya mwili yaliyoharibiwa vibaya.
Israel imetuma masanduku yenye 'mafuvu ya vichwa  na miili ya wanawake' ya Wapalestina huko Gaza
Corbyn alisema kuwa miongoni mwa mabaki hayo kulikuwa na miili ya wanawake. / AP
tokea masaa 6

Mbunge na kiongozi wa zamani wa Chama cha Labour nchini Uingereza, Jeremy Corbyn, ameeleza ujumbe alioupokea kutoka kwa mkurugenzi wa Hospitali ya Al-Shifa katika ukanda wa Gaza iliyozingirwa, ukihusu kuwasili kwa makumi ya masanduku yaliyokuwa na mafuvu na mabaki ya miili ya Wapalestina yaliyoharibiwa.

Corbyn alisema ujumbe kutoka kwa Dkt. Mohammed Abu Salmiya, ulieleza kuwa jeshi la Israel lilileta takribani masanduku 66 yenye mabaki ya miili ya binadamu katika hospitali hiyo.

Kulingana na Corbyn, wafanyakazi wa hospitali walipofungua masanduku hayo walikuta mafuvu ya Wapalestina waliouawa wakati wa mauaji ya halaiki.

Aidha, Corbyn alisema kuwa miongoni mwa mabaki hayo kulikuwa na miili ya wanawake waliokufa ambayo ilionyesha dalili za kufanyiwa upasuaji, jambo lililozua tuhuma kwamba viungo vya ndani vilikuwa vimetolewa.

“Ni vigumu kuelezea hili,” Corbyn aliongeza.

“Haya ndiyo yanayowatokea watu wa Palestina. Hii ni suala kubwa linalofafanua wakati huu wetu.”

Uharibifu wa miili na utoaji wa viungo vya ndani

Wizara ya Afya ya Gaza imethibitisha kupokea makumi ya miili na mabaki yasiyotambulika kupitia International Committee of the Red Cross (ICRC).

Maafisa wa afya waliokuwepo walisema baadhi ya mabaki hayo yalikuwa na “dalili zisizo za kawaida,” zikiwemo alama za upasuaji zinazoashiria uwezekano wa viungo kutolewa kabla ya miili kurejeshwa.

Dkt. Abu Salmiya, ambaye hapo awali aliwahi kushikiliwa na majeshi ya Israel, alieleza kuwa mabaki mengi hayakuweza kutambulika, yakijumuisha mifupa na mafuvu pekee.

Wizara ya Afya ilisema miili hiyo ilipokelewa ikiwa katika “hali ya kuharibiwa vibaya,” hali iliyofanya utambuzi kwa kutumia mbinu za kawaida za kitabibu kushindakana.

‘Palestina ndiyo changamoto kubwa ya wakati huu wetu’

Corbyn alifananisha kile alichokiita mauaji ya halaiki yanayofanywa na Israel na harakati za kihistoria za kupinga ufashisti katika karne ya 20.

“Nilipokuwa kijana, kadhia ya watu wengi ilikuwa ni maovu ya Vita vya Vietnam,” alisema, akilinganisha mshikamano wa kimataifa kwa Gaza na Brigedi za Kimataifa zilizopigana dhidi ya ufashisti nchini Hispania.

Siku ya Jumatatu, Corbyn alijiunga na waandamanaji nje ya Mahakama ya Westminster Magistrates’ Court kwa mshikamano na Ben Jamal, mkurugenzi wa Palestine Solidarity Campaign, pamoja na Chris Nineham wa Stop the War Coalition.

Wote wawili wanakabiliwa na mashtaka yanayohusiana na kuandaa maandamano ya amani tarehe 18 Januari 2025.

“Kuandamana kwa ajili ya Palestina si kosa la jinai,” Corbyn alisema nje ya mahakama.

Aliishutumu serikali kwa kujaribu “kuzuia haki ya kuandamana” na kuonya kuwa haki za msingi za kiraia, ikiwemo haki ya kuandamana “zinashambuliwa.”

CHANZO:TRT World