10 Septemba 2025
Akizungumza jijini Morogoro hivi karibuni wakati wa kampeni za kunadi sera zake, Mwiru amesema kuwa kuwa analenga kupambana na mafisadi, ikiwemo kupambana na kukomesha vitendo vya kifisadi nchini Tanzania.
“Ndugu zangu, kiama cha mafisadi kinakuja. Mkinachagua tarehe 29, Ikulu yangu kutakuwa na bwawa la kufuga mamba. Ikulu yangu itakuwa na bwawa la kufuga mamba. Huyo mamba ni kwa ajili ya kitanzi cha mafisadi,” alibainisha.