| Swahili
AFRIKA
2 DK KUSOMA
Kura za Senegal: Sall aonya dhidi ya kujitangazia ushindi
Rais wa Senegal Macky Sall amewaonya wagombea wa uchaguzi wa urais dhidi ya kujitangazia kushinda kabla matokeo rasmi kutolewa na tume.
Kura za Senegal: Sall aonya dhidi ya kujitangazia ushindi
Macky Sall anatarajiwa kujiuzulu kama rais wa Senegal mapema Aprili 2024. / Picha: Macky Sall / Others
25 Machi 2024

Rais anayemaliza muda wake wa Senegal Macky Sall amewaonya wagombea urais dhidi ya kutoa madai ya ushindi kabla ya wakati.

Si juu ya mgombea, wala kambi (ya kisiasa) kutangaza ushindi au matokeo," Sall alisema baada ya kupiga kura na mkewe katika mji wa magharibi wa kati wa Fatick siku ya Jumapili.

"Ni vituo vya kupigia kura ndivyo vitazungumza," Sall, ambaye hatagombea tena uchaguzi huo, aliongeza.

Wagombea 17 wa urais wanatafuta kumrithi Sall kama rais wa Senegal.

Zaidi ya raia milioni 7 wa Senegal walijiandikisha kama wapiga kura katika uchaguzi wa 2024, ambao ulicheleweshwa kwa utata kwa mwezi mmoja.

Mapema Februari, Sall alitangaza kwamba anaahirisha kwa muda usiojulikana uchaguzi wa urais wa Februari 25, lakini Baraza la Katiba la nchi hiyo lilimuamuru kufanya uchaguzi huo kabla ya kuondoka madarakani Aprili 2.

Pata habari zaidi kupitia Whatsapp channels

CHANZO:TRT Afrika