Settlers storm Al-Aqsa / Photo: مواقع تواصل

Zaidi ya watu 1,500 wa Israel wamevamia na kuingia katika eneo la Msikiti wa Al Aqsa Jerusalem Mashariki wakati wa likizo ya Kiyahudi ya Pasaka.

Katika taarifa, Idara ya Kiislamu mjini Jerusalem ilisema walowezi 1,532 walivamia Msikiti wa Al Aqsa siku ya Jumatatu.

Ilisema watu hao walivamia boma hilo wakiwa katika vikundi 21 wakisindikizwa na polisi wa Israel.

Hapo awali, polisi wa Israel waliwazuia Wapalestina walio na umri wa chini ya miaka 50 kuingia katika Msikiti wa Al Aqsa kuswali, mashahidi walisema.

Mashahidi hao walisema kuwa vikosi vya polisi viliwekwa Al Aqsa kabla ya kuruhusu makundi ya waisrael kuuvamia kupitia lango la Mughrabi kwenye ukuta wa magharibi wa msikiti huo.

Polisi pia waliwaondoa waumini kadhaa kutoka kwenye ua wa Msikiti wa Al Aqsa wakati wa uvamizi wa walowezi.

Siku ya Jumapili, Idara ya Kiislamu mjini Jerusalem ilisema walowezi 912 walivamia Msikiti wa Al Aqsa katika sikukuu ya Pasaka ya Kiyahudi, inayoendelea hadi Aprili 12.

TRT World