| swahili
UTURUKI
1 dk kusoma
Kauli maarufu za Erdogan zarindima jijini New York
Rais arudia wito wake wa mabadiliko kwenye Mkutano Mkuu wa Umoja wa Mataifa, akisema: “Ulimwengu ni mkubwa kuliko nchi tano.”
Kauli maarufu za Erdogan zarindima jijini New York
Ujumbe wa Erdogan wavuma jijini New York wakati wa Mkutano Mkuu wa Umoja wa Mataifa.
24 Septemba 2025

Picha ya Rais wa Uturuki, Recep Tayyip Erdogan, pamoja na kauli zake maarufu “Ulimwengu ni mkubwa kuliko nchi tano” na “Ulimwengu wa haki zaidi unawezekana” ziliwekwa kwenye barabara kuu na mitaa ya kati jijini New York.

Hizi ni kauli ambazo Erdogan amekuwa akizirudia kwa muda mrefu akitaka mabadiliko katika mfumo wa Umoja wa Mataifa.

Kwa miaka mingi, Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa limekosolewa kwa madai kuwa wanachama wake watano wenye kura ya turufu – Marekani, Uingereza, Ufaransa, Urusi na China – wana ushawishi mkubwa usio wa haki.

Akihutubia kikao cha 80 cha Mkutano Mkuu wa Umoja wa Mataifa siku ya Jumanne, Erdogan alisisitiza tena wito wake wa kutaka mabadiliko ndani ya Umoja huo.

“Ulimwengu wa haki zaidi unawezekana”

“Ninaamini kwa dhati kwamba ni jukumu letu sote kuchukua hatua zitakazoirudisha Umoja wa Mataifa kwenye misingi yake ya awali katika mwaka huu wa 80 tangu kuanzishwa kwake.

“Tutaendelea kusema, ‘Ulimwengu ni mkubwa kuliko nchi tano!’ hadi pale mfumo wa haki, na si wa nguvu pekee, utakapowekwa,” alisema.

Kauli yake “Ulimwengu wa haki zaidi unawezekana” pia ilionyeshwa kwenye skrini za LED katika eneo la Times Square jijini New York.

CHANZO:TRT World
Soma zaidi
Uturuki inamkumbuka Ataturk miaka 87 baada ya kufariki
Waziri wa mambo ya nje wa Uturuki kuzuru Marekani siku ya Jumatatu
Rais Erdogan anatumai Marekani itatimiza ahadi zake kuhusu makubaliano ya ndege za kivita za F-35
Palestina inapongeza amri za kukamatwa dhidi ya maafisa 37 wa Israel kutoka Uturuki kama 'ushindi
Ujumbe wa Erdogan 'Azerbaijan haiko peke yake' ulipelekea ushindi wa Karabakh: Aliyev
Ushindi wa Karabakh wa Azerbaijan kwa amani ya Caucasus: Rais Erdogan
Uturuki yatoa hati ya kukamatwa kwa Waziri Mkuu wa Israel Netanyahu, juu ya mashtaka ya mauaji
Erdogan: Uturuki kuharakisha miradi ya kiulinzi kuimarisha ‘maslahi’ na washirika wa Ulaya
Uturuki kuandaa mazungumzo ya Gaza wiki ijayo kufuatia wasiwasi juu ya usitishaji mapigano – Fidan
Mfumo wa ulimwengu wa sasa unazingatia nguvu zaidi ya haki: Mkurugenzi wa TRT
Israel imeigeuza Gaza kuwa vifusi, inawezaji kuwa haina hatia: Erdogan
Uturuki yakashifu unafiki wa nchi za Magharibi kuhusu Gaza, yatoa wito wa mfumo mpya wa dunia
Hamas haina nuyklia, Israel iko nayo: Erdogan aitaka Berlin ichukue hatua kali dhidi ya Tel Aviv
Erdogan ataka kuona mabadiliko katika uhusiano na EU na ushirikiano wa kikanda alipokutana na Mertz
Ujerumani yatoa wito wa kuunda “ushirikiano wa kimkakati” ili kukabiliana na changamoto za kimataifa
"Marekebisho ya Ulimwengu": Jukwaa la 9 la TRT World kuanza Istanbul likiangazia majadiliano na haki
Erdogan ametangaza washindi wa Tuzo Kuu za Utamaduni na Sanaa za Urais mwaka 2025
Uturuki yaadhimisha miaka 102 tangu kuanzishwa kwa Jamhuri
Uturuki yatoa wito wa kusitishwa mara moja kwa mapigano katika mji wa Al Fasher, Sudan
Uturuki na Jordan zasaini makubaliano ya kuimarisha uhusiano wa kiuchumi