| swahili
UTURUKI
2 dk kusoma
Uturuki inamkumbuka Ataturk miaka 87 baada ya kufariki
Rais wa Uturuki, viongozi wa vyama vya siasa, maafisa waandamizi wa mahakama, maafisa wa jeshi, watumishi wengine wa serikali walikusanyika Anitkabir jijini Ankara kumkumbuka Mustafa Kemal Ataturk, muasisi na rais wa kwanza wa nchi.
Uturuki inamkumbuka Ataturk miaka 87 baada ya kufariki
Erdogan aliweka mashada ya maua mekundu na meupe yenye muundo wa bendera ya Uturuki katika kaburi la Ataturk.
10 Novemba 2025

Mustafa Kemal Ataturk, muasisi wa Jamhuri ya Uturuki, alikumbukwa siku ya Jumatatu miaka 87 tangu alipofariki kwa hafla rasmi ya kitaifa Anitkabir, makumbusho alipozikwa katika mji mkuu Ankara.

Hafla hiyo ilianza kwa kushiriki kwa Rais Recep Tayyip Erdogan, Spika wa Bunge Numan Kurtulmus, mawaziri, viongozi wa vyama vya kisiasa, maafisa waandamizi wa mahakama, na makamanda wa kijeshi.

Erdogan aliweka mashada ya maua mekundu na meupe yaliyowekwa kwa muundo wa bendera ya Uturuki katika kaburi la Ataturk.

Saa tatu na dakika tano asubuhi, muda hasa aliofariki Ataturk, walioshiriki walikaa kimya kwa muda, na baadaye kuimbwa wimbo wa taifa. Wakati wa kutoa heshima, bendera ya Uturuki ilishushwa nusu mlingoti.

Baadaye, Erdogan na maafisa aliyoandamana nao walielekea katika eneo la Misak-i Milli, ambapo alitia saini Kitabu cha Kumbukumbu cha Anitkabir, akitoa heshima zake kwa Ataturk na wenzake waliopigania taifa.

"Kwa dhati kabisa tunalinda Jamhuri ya Uturuki, ambayo uliiita kuwa 'kazi kubwa,' na kuendelea kupamba kila sehemu ya nchi yetu na mafanikio mapya," Erdogan aliandika.

"Chini ya uongozi thabiti na viongozi waliobobea, Uturuki inaimarika na kwa ujasiri ili kuwa nchi yenye uwezo duniani," aliongeza.

Ataturk alikuwa rais wa kwanza wa jamhuri hadi Novemba 10, 1938, alipofariki jijini Istanbul akiwa na umri wa miaka 57 kutokana na maradhi ya ini.

Kwa kawaida watu wa Uturuki hutembelea kaburi lake kila Novemba 10 kutoa heshima zao kwa muasisi wa taifa.

CHANZO:AA
Soma zaidi
Uturuki inaangazia ushirikiano na ujumuishi katika nia ya kuandaa mkutano wa COP31
Uturuki inakaribisha makubaliano ya amani kati ya serikali ya DRC na waasi wa M23
Uungwaji mkono wa Ujerumani unaashiria 'upya wa nia ya kisiasa' kwa ombi la Uturuki la EU: Fidan
Fidan: Njia ya kusuluhisha vikwazo vya Marekani iko wazi huku Trump akionyesha nia yake
Rais Erdogan aadhimisha kumbukumbu ya miaka 42 ya kuanzishwa kwa TRNC
Rais Erdogan afungua maonyesho ya 'Echoes' Istanbul kwa heshima ya Sule Yuksel Senler na Malcolm X
Uturuki yaadhimisha miaka 81 ya kupelekwa uhamishoni Waturuki wa Ahiska kutoka Georgia
Hafla yafanyika Uturuki ya kuwakumbuka wanajeshi waliofariki kwenye ajali ya ndege
Wanajeshi 20 wa Uturuki wafariki katika ajali ya ndege ya mizigo ya kijeshi huko Georgia: wizara
Wanajeshi 20 wa Uturuki wauawa katika ajali ya ndege ya shehena ya kijeshi huko Georgia: wizara
Ndege ya kijeshi ya mizigo ya Uturuki yaanguka mpakani mwa Georgia na Azerbaijan ikiwa na watu 20
Uimarishaji wa Uturuki ni heshima na kumuenzi Ataturk: Erdogan
Waziri wa mambo ya nje wa Uturuki kuzuru Marekani siku ya Jumatatu
Rais Erdogan anatumai Marekani itatimiza ahadi zake kuhusu makubaliano ya ndege za kivita za F-35
Palestina inapongeza amri za kukamatwa dhidi ya maafisa 37 wa Israel kutoka Uturuki kama 'ushindi
Ujumbe wa Erdogan 'Azerbaijan haiko peke yake' ulipelekea ushindi wa Karabakh: Aliyev
Ushindi wa Karabakh wa Azerbaijan kwa amani ya Caucasus: Rais Erdogan
Uturuki yatoa hati ya kukamatwa kwa Waziri Mkuu wa Israel Netanyahu, juu ya mashtaka ya mauaji
Erdogan: Uturuki kuharakisha miradi ya kiulinzi kuimarisha ‘maslahi’ na washirika wa Ulaya
Uturuki kuandaa mazungumzo ya Gaza wiki ijayo kufuatia wasiwasi juu ya usitishaji mapigano – Fidan