24 Desemba 2025
Miongoni mwa waliofariki pamoja na al-Haddad ni Kamanda wa Kikosi cha Ardhini, Brigedia Jenerali na mpiga picha wa ofisi ya vyombo vya habari vya jeshi.
Katika taarifa yake, ubalozi wa Uturuki ulisema kuwa umehuzunishwa sana na vifo hivyo.
ZILIZOPENDEKEZWA
"Tunaomba Mungu awarahemu waliofariki na tunatoa rambirambi zetu pamoja na dua za kuwapapa subira kwa Serikali ya Umoja wa Kitaifa, wananchi wote wa Libya, familia zao na wenzao katika jeshi," ilisema taarifa hiyo.
Mabaki ya ndege binafsi ya Falcon 50 yalipatikana na maafisa wa usalama wa Uturuki katika wilaya ya Haymana karibu na Ankara, kulingana na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Uturuki.
CHANZO:TRT Arabi, TRT Afrika



























