| Swahili
UTURUKI
2 dk kusoma
Uwanja wa ndege wa Sabiha Gökçen umehudumia abiria milioni 44.2 katika kipindi cha miezi 11
Kwa mujibu wa maafisa, idadi ya abiria iliongezeka kwa asilimia 31 katika miezi 11 ya mwaka 2025 ikilinganishwa na kipindi cha kabla ya njia ya pili ya ndege kuanza kutumika mwaka 2023.
Uwanja wa ndege wa Sabiha Gökçen umehudumia abiria milioni 44.2 katika kipindi cha miezi 11
"Katika muda wa miezi 11 tu, tulipita rekodi ya abiria milioni 41.4 ya mwaka wa 2024," taarifa rasmi. / / AP
26 Desemba 2025

Uwanja wa Ndege wa Sabiha Gökçen, ambao ni kituo cha usafiri wa anga upande wa Asia wa jiji la Istanbul, ulihudumia abiria milioni 44.2 kati ya Januari na Novemba, na kuvunja rekodi ya mwaka uliopita ya abiria milioni 41.4.

Waziri wa Uchukuzi na Miundombinu wa Uturuki, Abdulkadir Uraloğlu, alisema Alhamisi kuwa njia mpya ya ndege, iliyofunguliwa Desemba 2023 ili kuruhusu ndege kubwa kutua, imechangia kwa kiasi kikubwa kufikiwa kwa rekodi hiyo.

Taarifa hiyo ilitolewa katika maadhimisho ya miaka miwili tangu njia hiyo mpya ya ndege ianze kufanya kazi.

Uraloğlu alisema kuwa, pamoja na njia hiyo mpya, miundombinu mingine kama njia za kupitisha ndege (taxiway), maeneo ya maegesho ya ndege zenye uwezo mkubwa na mizigo, mnara wa kudhibiti safari za ndege, pamoja na majengo ya kisasa, vimeongeza kwa kiasi kikubwa uwezo wa uwanja wa ndege wa Sabiha Gökçen kuhudumia safari za anga.

Mwaka 2023, jumla ya abiria milioni 33.7 walihudumiwa kwenye safari za ndani na za kimataifa kati ya Januari na Novemba.

“Idadi ya abiria iliongezeka kwa asilimia 31 katika miezi 11 ya mwaka 2025 ikilinganishwa na kipindi cha kabla ya njia ya pili ya ndege kuanza kufanya kazi mwaka 2023,” alisema.

“Ndani ya miezi 11 pekee, tulipita rekodi ya abiria milioni 41.4 iliyofikiwa katika mwaka mzima wa 2024,” aliongeza.

Uraloğlu pia alisema kulikuwa na safari za ndege 208,643 kati ya Januari na Novemba 2023, na idadi hiyo ikaongezeka kwa asilimia 20 hadi kufikia 250,538 katika kipindi hicho hicho mwaka huu. Aliongeza kuwa, “Kwa mwaka mzima wa 2024, idadi hiyo ilikuwa ndege 242,612.”

CHANZO:AA
Soma zaidi
Uturuki yafichua maelezo ya mpango wa uchimbaji visima pwani ya Somalia
Waliowasababishia mateso watu wa Gaza ‘watawajibishwa’: Erdogan
Shirika la Ndege la Uturuki kujenga kituo kikubwa zaidi cha mizigo kwa zaidi ya bilioni $2.3
Fidan na Kalin wa Uturuki wakutana na Umerov wa Ukraine jijini Ankara
Zaidi ya watu 500,000 waandamana kuiunga mkono Palestina mjini Istanbul katika siku ya Mwaka Mpya
Uturuki kuruhusu viza bila malipo kwa raia wa China
Uturuki kuendeleza juhudi za amani na diplomasia mwaka 2026: Fidan
Uturuki haitakubali uchokozi katika eneo la Mediterania ya Mashariki: Rais Erdogan
Uturuki yaanza ujenzi wa kituo cha anga ya juu nchini Somalia: Waziri
Somalia inapongeza mkataba wa kuchimba mafuta na Uturuki kabla ya shughuli za baharini za 2026
Uturuki yapinga hatua ya Israel kuhusu Somaliland, yaahidi kuimarisha ushirikiano na Somalia
Balozi wa Somalia nchini Uturuki anapongeza uungwaji mkono wa serikali ya Uturuki
Uturuki na Armenia zakubaliana kurahisisha utoaji wa viza katika jitihada za kuimarisha uhusiano
Rais wa Uturuki apongeza 'juhudi za ujenzi mpya' wakati wa utoaji wa nyumba za waathiriwa 455,000
Jamii ya Waturuki yafungua msikiti mpya nchini Uganda
Uturuki inazindua mpango wa kwanza wa kitaifa wa kujiandaa na maafa kwa watoto
Uturuki inafanya maombi mjini Ankara kwa ajili ya wajumbe wa Libya waliofariki
Uturuki inalaani Israel kwa kutambua Somaliland
Wachunguzi wapekua eneo la ajali ya ndege iliyomuua Mkuu wa Jeshi la Libya
Ubalozi wa Uturuki unaomboleza kifo cha Mkuu wa Jeshi wa Libya