| swahili
AFRIKA
2 dk kusoma
Baraza la Maaskofu Tanzania lataka uwajibikaji kwa waliohusika na mauaji ya waandamanaji
Maaskofu wa Tanzania wamelaani mauaji hayo na kuitisha uchunguzi unaoshirikisha wadau wa ndani na wa nje huku wakiiomba serikali iwe tayari kutekeleza ripoti itakayotolewa
Baraza la Maaskofu Tanzania lataka uwajibikaji kwa waliohusika na mauaji ya waandamanaji
Wakuu wa vyombo vya ulinzi na usalama na wote waliohusika na mauaji WAWAJIBIKE au KUWAJIBISHWA na mamlaka zao za uteuzi. / Ukurasa wa X
15 Novemba 2025

Baraza la Maaskofu Tanzania limelaani vikali mauaji ya waandamanaji wakati na baada ya uchaguzi mkuu kama uovu mkubwa na chukizo kwa Mungu.

Kupitia kwa Rais wa Baraza hilo na Askofu wa Jimbo Katoliki la Lindi, Mhashamu Wolfgang Pisa baraza hilo limesisitiza kuwa maandamano ni haki na sio kila mandamano ni uhalifu.

‘‘Kuandamana ni haki ya raia kama njia ya kufikisha ujumbe au malalamiko ikiwa njia ya mazungumzo imeshindikana chamsingi yawe maandamano ya amani,’’ ilisem ataarifa hiyo. ‘‘Inasikitisha kuona kuwa Waandamanaji waliojitokeza siku ya uchaguzi wote waliwekwa katika mwavuli wa uhalifu. Adhabu ya mwandamanajii siyo kuuawa.’’ iliendelea kusema taarifa.

Baraza hilo limekariri baadhi ya malalamiko ya muda mrefu kutoka kwa baadhi ya raia kuhusu matukio ya waziwazi ya mauaji, utekaji, kupigwa na kuumizwa kwa raia.

Sababu zilizochangia maandamano

Serikali imekuwa ikikanusha madai haya japo vyombo vya usalama vimetoa taarifa ya kufanyia uchunguzi visa maalum vilivyotajwa vya utekaji.

Maaskofu hao wameelezea sababu kadhaa wanazoamini zilichangia kuzuka maandamano na rabsha ikiwemo kudorora usalama, kukiukwa taratibu za demokrasia juu ya kuwachagua viongozi na ukosefu wa usikizi kwa malalamiko ya wananchi.

Baraza hilo la Maaskofu limeorodhesha matakwa yao katika taarifa hiyo ikiwemo kuwataka wakuu wa vyombo vya ulinzi na usalama na wote waliohusika na mauaji wawajibike au kuwajibishwa na mamlaka zao za uteuzi.

Katika orodha ya vitu vinane walivyotaka vifanyike, pia wameitisha wale wote waliokamatwa kwa hila kabla na baada ya uchaguzi na kuwekwa mahabusu au mahali pasipojulikana waachiwe huru na bila ya masharti yoyote.

Tume ya kuchunguza mauaji

‘‘Katiba mpya na utawala wa sheria vimekuwa kilio cha muda mrefu hapa nchini. Mchakato wa Katiba mpya yenye kujali utu, usawa, haki, ukweli kwa wote uanze kwa kukushirikisha wadau wote. Ili tusirudi tena katika machafuko na nchi iongozwe katika utawala wa sheria.’’ wameongeza.

Tanzania imetumbukia katika lawama na shutuma za kimataifa tangu Oktoba 29, ambapo maandamano ya kupinga uchaguzi mkuu yalikabiliwa kwa nguvu kupita kiasi, huku vijana wengi wakidaiwa kuuawa kw akupigwa risasi na vyombo vya uslama.

Awali uongozi wa serikali ulikanusha madai kuwa Watanzania waliuawa, lakini baadaye, katika hotuba ya kwanz aya kulifungua bunge Rais Samia Suluhu Hassan, alitangaza kuteua tume itakayofanya uchunguzi huku akitoa pole kwa waliofiwa na waliojeruhiwa katika maandamano.

CHANZO:TRT Afrika Swahili
Soma zaidi
Cape Verde, Mauritius na Ushelisheli wafanikiwa kuangamiza surua na  rubela
Rais wa Sudan Kusini Kiir amrejesha makamu wa rais katika mabadiliko ya baraza la mawaziri
Zaidi ya watu 100,000 wamekimbia makazi yao kutoka Al Fasher ya Sudan tangu kutwaliwa na RSF
Rais wa Tanzania amteua binti na mkwe wake katika Baraza la Mawaziri
Rais Samia amteua waziri mpya wa fedha, awaacha mawaziri wa mambo ya nje na madini madarakani
Tovuti za taasisi za serikali ya Kenya zashambuliwa
Mgodi waporomoka DRC na kuua watu wasiopungua 32
Wahamiaji 4 wafariki baada ya boti mbili zilizokuwa zimebeba makumi ya watu kuzama pwani ya Libya
Kikundi cha matabibu kinaripoti visa ya ubakaji wa wasichana wa Al Fasher baada ya RSF kuteka
Mlipuko wa virusi vya Marburg umethibitishwa kusini mwa Ethiopia
DR Congo, M23 wasaini makubaliano ya amani 'ya kihistoria' nchini Qatar
Baraza la usalama la UN laongezea mwaka mmoja ujumbe wa amani wa Abyei
Kiongozi wa zamani wa waasi wa DRC anayeshtakiwa Paris kwa uhalifu wa kivita aanza mgomo wa kula
UN yaagiza uchunguzi wa dharura ufanyike kuhusu ukiukaji wa sheria katika Al Fasher ya Sudan
Rais wa Tanzania atangaza uchunguzi kuhusu mauaji ya waandamanaji katika uchaguzi
Wakimbizi 57,000 wamewasili kaskazini mwa Sudan baada ya mashambulizi ya RSF huko Darfur, Kordofan
Afrika Kusini yaruhusu kuingia kwa wakimbizi zaidi ya 150 kutoka Gaza, Palestina
Afrika yakumbwa na mlipuko wa kipindupindu mbaya zaidi katika miaka 25
Mataifa ya G7 walaani mashambulizi ya RSF dhidi ya raia Sudan, watoa wito wa kusitishwa mapigano
Wakenya zaidi ya 200 wajiunga na jeshi la Urusi