| Swahili
UTURUKI
2 dk kusoma
Erdogan kwa Trump: Venezuela isiingizwe katika hali ya kutokuwa na usalama
Rais wa Uturuki ameeleza msimamo wa Uturuki kuwaunga mkono "watu wa Venezuela marafiki katika kupambania mafanikio, amani, na ustawi."
Erdogan kwa Trump: Venezuela isiingizwe katika hali ya kutokuwa na usalama
Rais wa Uturuki Recep Tayyip Erdogan. / AA
6 Januari 2026

Rais wa Uturuki Tayyip Erdogan amesema kuwa amemwambia Rais wa Marekani Donald Trump katika mazungumzo kwa njia ya simu kwamba Venezuela haitakiwi kuingizwa katika hali ya kutokuwa na usalama baada ya kumpindua kiongozi wake Nicolas Maduro.

Akizungumza baada ya mkutano wa baraza la mawaziri siku ya Jumatatu, Erdogan alionya kuwa kukiuka uhuru wa nchi na kudharau sheria za kimataifa ni hatari sana na huenda kukasababisha “matatizo makubwa duniani.”

“Uturuki haiungi mkono hatua zozote za ukiukwaji wa sheria ya kimataifa,” Erdogan alisema, akiongeza kuwa Uturuki inajitahidi kufanya kile kilicho bora kwa Uturuki na “taifa la ndugu zetu wa Venezuela.”

Amesema Uturuki inaunga mkono “watu wa Venezuela marafiki katika kupambania mafanikio, amani na ustawi,” akieleza kuwa Maduro na watu wa Venezuela waliwahi kuonesha urafiki kwa Uturuki hapo awali.

Erdogan pia alisisitiza umuhimu wa kuzingatia sheria za utawala za kimataifa.

Uturuki iko "mstari wa mbele" kwa nchi kote duniani ambazo zinatetea haki, uhalali, na sheria ya kimataifa, alisema.

Marekani ilimteka nyara Maduro na mkewe mapema siku ya Jumamosi kutoka nyumbani kwao katika kambi ya kijeshi na kuwaweka kwenye meli ya kivita ya Marekani kwa ajili ya kushtakiwa jijini New York wakiwashtumu kwa kuhusika na njama ya ugaidi wa mihadarati.

Maduro alionekana kwa mara ya kwanza katika mahakama ya Manhattan siku ya Jumatatu, ambapo alikanusha mashtaka yote ya Marekani.

Kuondolewa kwake kunakuja baada ya Marekani kwa miezi kadhaa kupeleka wanajeshi wengi pwani ya karibu na Venezuela na madai ya kulipua maboti yaliyokuwa yakisafirisha dawa za kulevya.

Trump amesisitiza kuwa Marekani itasimamia utawala wa Venezuela kwa muda na kuuza mafuta ya nchi hiyo kwa mataifa mengine.

CHANZO:TRT World
Soma zaidi
Shirika la Ndege la Uturuki kujenga kituo kikubwa zaidi cha mizigo kwa zaidi ya bilioni $2.3
Fidan na Kalin wa Uturuki wakutana na Umerov wa Ukraine jijini Ankara
Zaidi ya watu 500,000 waandamana kuiunga mkono Palestina mjini Istanbul katika siku ya Mwaka Mpya
Uturuki kuruhusu viza bila malipo kwa raia wa China
Uturuki kuendeleza juhudi za amani na diplomasia mwaka 2026: Fidan
Uturuki haitakubali uchokozi katika eneo la Mediterania ya Mashariki: Rais Erdogan
Uturuki yaanza ujenzi wa kituo cha anga ya juu nchini Somalia: Waziri
Somalia inapongeza mkataba wa kuchimba mafuta na Uturuki kabla ya shughuli za baharini za 2026
Uturuki yapinga hatua ya Israel kuhusu Somaliland, yaahidi kuimarisha ushirikiano na Somalia
Balozi wa Somalia nchini Uturuki anapongeza uungwaji mkono wa serikali ya Uturuki
Uturuki na Armenia zakubaliana kurahisisha utoaji wa viza katika jitihada za kuimarisha uhusiano
Rais wa Uturuki apongeza 'juhudi za ujenzi mpya' wakati wa utoaji wa nyumba za waathiriwa 455,000
Jamii ya Waturuki yafungua msikiti mpya nchini Uganda
Uturuki inazindua mpango wa kwanza wa kitaifa wa kujiandaa na maafa kwa watoto
Uturuki inafanya maombi mjini Ankara kwa ajili ya wajumbe wa Libya waliofariki
Uturuki inalaani Israel kwa kutambua Somaliland
Uwanja wa ndege wa Sabiha Gökçen umehudumia abiria milioni 44.2 katika kipindi cha miezi 11
Wachunguzi wapekua eneo la ajali ya ndege iliyomuua Mkuu wa Jeshi la Libya
Ubalozi wa Uturuki unaomboleza kifo cha Mkuu wa Jeshi wa Libya
Wachunguzi wa Uturuki wapekua eneo la ajali ya ndege iliyomuua Mkuu wa Jeshi la Libya