| Swahili
AFRIKA
1 dk kusoma
Jeshi la Polisi Tanzania lakiri kumshikilia aliyekuwa Waziri wa Uwekezaji Geofrey Mwambe
Kulingana na taarifa yake iliyotolewa Disemba 12, 2025, jeshi hilo limesema kuwa lilimkamata Mwambe Disemba 7, 2025 katika eneo la Tegeta wilaya ya Kinondoni.
Jeshi la Polisi Tanzania lakiri kumshikilia aliyekuwa Waziri wa Uwekezaji Geofrey Mwambe
Geofrey Mwambe/Picha:Wengine / Others
tokea masaa 13

Jeshi la Polisi Kanda Maalumu ya limesema kuwa limemkamata na linaendelea kumshikilia aliyekuwa Waziri wa Uwekezaji na Mbunge wa Masasi, Geofrey Mwambe kwa tuhuma za jinai ambazo zinachunguzwa.

Kulingana na taarifa yake iliyotolewa Disemba 12, 2025, jeshi hilo limesema kuwa lilimkamata Mwambe Disemba 7, 2025 katika eneo la Tegeta wilaya ya Kinondoni.

Aidha, taarifa hiyo imeongeza kuwa Mwambe, ambaye amewahi kuwa Mkurugenzi wa Kituo cha Uwekezaji nchini humo (TIC), amekamatwa kwa tuhuma za makosa ya jinai.

“Hatua zaidi za kisheria zinakamilishwa,” ilisomeka sehemu ya taarifa hiyo.

Geoffrey Mwambe amewahi kuwa Waziri wa Viwanda na Biashara  kuanzia mwaka 2020 hadi 2021, akateuliwa tena kuwa kuwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Uwekezaji), kuanzia mwaka 2021 hadi 2022.

CHANZO:TRT Afrika Swahili