| swahili
UTURUKI
1 dk kusoma
Trump, Erdogan waahidi ushirikiano wa karibu zaidi, waangazia mauzo ya ndege za kivita na biashara
Trump amempongeza rais wa Uturuki akimtaja kuwa "mtu anayeheshimika sana", akisema kuwa Erdogan anapendwa "sana katika nchi yake na kote barani Ulaya, na duniani kote".
Trump, Erdogan waahidi ushirikiano wa karibu zaidi, waangazia mauzo ya ndege za kivita na biashara
Trump anasema yeye na Erdogan watajadili kuhusu manunuzi ya Uturuki ya ndege za kivita za Marekani, ikiwemo F-16 na F-35. / AP
25 Septemba 2025

Rais wa Marekani Donald Trump na Rais wa Uturuki Recep Tayyip Erdogan wameapa kuimarisha ushirikiano kuhusu masuala ya ulinzi na biashara wakati wa mazungumzo yao katika Ikulu ya Marekani ya White House siku ya Alhamisi.

Trump amesema kuwa yeye na Erdogan watajadili kuhusu Uturuki kununua ndege za kivita zilizotengenezwa Marekani, ikiwemo F-16 na F-35, pamoja na ushirikiano wa kiuchumi.

“Tutatia saini makubaliano muhimu kwa nchi zetu zote mbili,” Trump aliwaambia waandishi wa habari, akiongeza kuwa vikwazo kwa Uturuki kuhusu kununua mifumo ya makombora kutoka kwa Urusi huenda vikaondolewa “mara moja”.

Akiwa amekaa pembeni mwa Trump katika ofisi ya rais ya Oval, Erdogan alisema majadiliano yataangazia masuala mbalimbali, ikiwemo mauzo ya ulinzi.

“Tuko katika mchakato tofauti wa uhusiano wa Uturuki na Marekani,” alisema. “Naamini kwa pamoja, mkono kwa mkono, tutaweza kukabiliana na hizi changamoto katika kanda.”

Trump alimpongeza mwenzake kuwa “mtu ambaye anaheshimika sana”, akisema Erdogan anapendwa “sana nchini kwake na kote barani Ulaya, na duniani kote”.

Mkutano huu unakuja baada ya tofauti za muda mrefu kujitokeza kati ya washirika wa NATO kuhusu manunuzi ya kijeshi, mapigano katika kanda na vikwazo vya kifedha, lakini viongozi wote walionekana kufikia muafaka, na kusisitiza ushirikiano kuliko makabiliano.

CHANZO:TRT World
Soma zaidi
Uturuki inamkumbuka Ataturk miaka 87 baada ya kufariki
Waziri wa mambo ya nje wa Uturuki kuzuru Marekani siku ya Jumatatu
Rais Erdogan anatumai Marekani itatimiza ahadi zake kuhusu makubaliano ya ndege za kivita za F-35
Palestina inapongeza amri za kukamatwa dhidi ya maafisa 37 wa Israel kutoka Uturuki kama 'ushindi
Ujumbe wa Erdogan 'Azerbaijan haiko peke yake' ulipelekea ushindi wa Karabakh: Aliyev
Ushindi wa Karabakh wa Azerbaijan kwa amani ya Caucasus: Rais Erdogan
Uturuki yatoa hati ya kukamatwa kwa Waziri Mkuu wa Israel Netanyahu, juu ya mashtaka ya mauaji
Erdogan: Uturuki kuharakisha miradi ya kiulinzi kuimarisha ‘maslahi’ na washirika wa Ulaya
Uturuki kuandaa mazungumzo ya Gaza wiki ijayo kufuatia wasiwasi juu ya usitishaji mapigano – Fidan
Mfumo wa ulimwengu wa sasa unazingatia nguvu zaidi ya haki: Mkurugenzi wa TRT
Israel imeigeuza Gaza kuwa vifusi, inawezaji kuwa haina hatia: Erdogan
Uturuki yakashifu unafiki wa nchi za Magharibi kuhusu Gaza, yatoa wito wa mfumo mpya wa dunia
Hamas haina nuyklia, Israel iko nayo: Erdogan aitaka Berlin ichukue hatua kali dhidi ya Tel Aviv
Erdogan ataka kuona mabadiliko katika uhusiano na EU na ushirikiano wa kikanda alipokutana na Mertz
Ujerumani yatoa wito wa kuunda “ushirikiano wa kimkakati” ili kukabiliana na changamoto za kimataifa
"Marekebisho ya Ulimwengu": Jukwaa la 9 la TRT World kuanza Istanbul likiangazia majadiliano na haki
Erdogan ametangaza washindi wa Tuzo Kuu za Utamaduni na Sanaa za Urais mwaka 2025
Uturuki yaadhimisha miaka 102 tangu kuanzishwa kwa Jamhuri
Uturuki yatoa wito wa kusitishwa mara moja kwa mapigano katika mji wa Al Fasher, Sudan
Uturuki na Jordan zasaini makubaliano ya kuimarisha uhusiano wa kiuchumi