| Swahili
ULIMWENGU
1 dk kusoma
Jenerali mwandamizi wa Urusi auawa katika shambulio la gari Moscow
Jenerali mwandamizi wa jeshi la Urusi ameuawa katika shambulio la bomu la gari jijini Moscow, huku wachunguzi wakifuatilia nadharia mbalimbali, ikiwa ni pamoja na uwezekano wa kuhusika kwa idara za kijasusi za Ukraine.
Jenerali mwandamizi wa Urusi auawa katika shambulio la gari Moscow
Mpelelezi anachunguza eneo ambalo jenerali mkuu wa Urusi aliripotiwa kuuawa kwa bomu lililotegwa kwenye gari huko Moscow, Urusi, Desemba 22, 2025. / / Reuters
22 Desemba 2025

Luteni Jenerali Fanil Sarvarov, afisa wa juu wa kijeshi, alifariki dunia baada ya kilipuzi kulipuka chini ya gari lake asubuhi ya Jumatatu, kwa mujibu wa Kamati ya Uchunguzi ya Urusi.

Katika taarifa iliyotolewa kupitia jukwaa la mawasiliano la Telegram, kamati hiyo ilisema kuwa Luteni Jenerali Sarvarov, ambaye alikuwa mkuu wa Idara ya Mafunzo ya Kiutendaji ya Makao Makuu ya Jeshi la Urusi, alikufa kutokana na majeraha yaliyosababishwa na mlipuko huo.

“Kwa mujibu wa wachunguzi, asubuhi ya Desemba 22, kilupizi kilichokuwa kimetegwa chini ya gari kililipuliwa katika Mtaa wa Yasenevaya jijini Moscow,” ilisema taarifa hiyo.

Kamati hiyo iliongeza kuwa uchunguzi umeanzishwa rasmi kufuatia kufunguliwa kwa kesi ya jinai mjini Moscow. Wachunguzi wanasema wanaendelea kuchunguza nadharia mbalimbali kuhusu mauaji hayo, ikiwa ni pamoja na uwezekano wa kuhusika kwa idara za kijasusi za Ukraine.

Hadi sasa, mamlaka za Ukraine bado hazijatoa ufafanuzi wowote kuhusu madai hayo.

CHANZO:AA
Soma zaidi
Hofu yaongezeka miongoni mwa jamii ya Wasomali baada ya Trump kutuma maafisa 2,000 Minnesota
Trump atishia shambulio la pili Venezuela, aonya kuhusu operesheni nyingine Colombia
Dunia imepokea vipi shambulio la Marekani nchini Venezuela?
Mashambulizi ya Marekani nchini Venezuela yaliua takriban watu 40: ripoti
Mwanabondia Anthony Joshua arejea Uingereza baada ya ajali ya gari Nigeria
Je, ajenda ya Marekani kubadili mfumo itafanikiwa Venezuela?
Shutuma za kimataifa zaongezeka kutokana na mashambulizi ya Marekani dhidi ya Venezuela
Rais Maduro na mkewe wamelazimika kuondoka Venezuela, anasema Trump
Milipuko yatikisa Caracas kufuatia onyo la Trump la kushambulia Venezuela
Venezuela yawaachia wafungwa 88 wa maandamano ya baada ya uchaguzi
Maelfu waandamana jijini Istanbul kuunga mkono Wapalestina
Israel inataka kufuta vibali vya mashirika ya misaada Gaza na Ukingo wa Magharibi
Watu 6 wameuawa Syria kufuatia shambulio la msikitini wakati wa swala ya Ijumaa
Papa Leo azungumzia madhila ya Gaza katika mahubiri ya Krismasi yake ya kwanza
Papa Leo aadhimisha mkesha wa Krismasi kwa mara ya kwanza kama Baba Mtakatifu
Ubelgiji yajiunga katika kesi ya mauaji ya halaiki ya Afrika Kusini dhidi ya Israel
Marekani yatoa ofa ya $3000 kwa wahamiaji kujiondoa nchini, nyongeza ya mara tatu
Trump awafuta kazi mabalozi 30 wa Marekani katika msukumo wa ajenda ya 'Amerika Kwanza'
Elon Musk anakuwa bilionea wa kwanza duniani wa $700b baada ya mkataba wa malipo wa Tesla kurejeshwa
Israel yashambulia kwa mabomu harusi ya Gaza na kuua Wapalestina 6 licha ya makubaliano ya amani