AFRIKA
1 dk kusoma
Hemed Suleiman ‘Morocco’ kutoipeleka Tanzania AFCON Morocco
Nafasi ya kocha huyo kwa sasa inachukuliwa na mzawa Miguel Gamondi, raia wa Argentina ambaye alikuwa akiifundisha Singida Big Stars ya nchini Tanzania.
Hemed Suleiman ‘Morocco’ kutoipeleka Tanzania AFCON Morocco
Miguel Gamondi akiwa mazoezini na kikosi cha Singida Big Stars./Picha:Wengine
tokea masaa 7

Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limesitisha mkataba wa Kocha Mkuu wa timu ya Taifa ya Tanzania ‘Taifa Stars’, Hemed Suleiman ‘Morocco’.

Kulingana na taarifa iliyotolewa na Novemba 4, 2025 na shirikisho hilo, mkataba huo umesitishwa kwa makubaliano ya pande mbili, yaani TFF kwa upande mmoja na Kocha Morocco kwa upande mwingine.

Kutokana na hatua hiyo, TFF imemteua Kocha Miguel Gamondi wa timu ya Singida Black Stars kuwa Kaimu Kocha Mkuu wa Taifa Stars.

Rais huyo wa Argentina anatarajiwa kuiongoza Taifa Stars kwenye Fainali za AFCON zitakazofanyika nchini Morocco, kuanzia Disemba 2025.