| swahili
UTURUKI
1 dk kusoma
Rais Erdogan ataka mageuzi Umoja wa Mataifa alipokutana Katibu Mkuu Guterres
Rais wa Uturuki, Recep Tayyip Erdogan, amesisitiza haja ya kufanyika kwa mageuzi katika mfumo wa Umoja wa Mataifa (UN), akisema kuwa Uturuki iko tayari kuchangia katika mchakato huo.
Rais Erdogan ataka mageuzi Umoja wa Mataifa alipokutana Katibu Mkuu Guterres
Mkutano huo ulizungumzia masuala ya kikanda na kimataifa, hususan mashambulizi ya Israel dhidi ya Gaza. /
24 Septemba 2025

Katika mkutano wake na Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Antonio Guterres, uliofanyika Jumanne jijini New York, Erdogan alisema kuwa haja ya marekebisho katika mfumo wa UN imejitokeza wazi katika miaka ya hivi karibuni.

Kwa mujibu wa taarifa ya Kurugenzi ya Mawasiliano ya Uturuki, mazungumzo yao yalijikita katika masuala ya kikanda na kimataifa, hasa mashambulizi ya Israel dhidi ya Gaza.

Erdogan alisema kuwa Uturuki itaendelea kutoa kila aina ya mchango katika juhudi za mageuzi, na kwamba umuhimu wa kulinda amani ya dunia umeeleweka zaidi kutokana na changamoto ambazo dunia imekumbana nazo katika miaka ya hivi karibuni.

Alieleza kuwa uchokozi wa Israel hauwalengi tu Wapalestina, bali pia unahatarisha amani ya kikanda na ya kimataifa. Alitoa wito kwa jumuiya ya kimataifa kuongeza shinikizo kwa Israel ili kuhakikisha misaada ya kibinadamu inawafikia watu wa Gaza bila vikwazo.

Aidha, Erdogan alisema kuwa Uturuki inazidisha juhudi zake za kukomesha vita kati ya Urusi na Ukraine, akisisitiza umuhimu wa usitishaji mapigano wa haraka na upatikanaji wa amani ya kudumu.

 

CHANZO:AA
Soma zaidi
Uturuki inamkumbuka Ataturk miaka 87 baada ya kufariki
Waziri wa mambo ya nje wa Uturuki kuzuru Marekani siku ya Jumatatu
Rais Erdogan anatumai Marekani itatimiza ahadi zake kuhusu makubaliano ya ndege za kivita za F-35
Palestina inapongeza amri za kukamatwa dhidi ya maafisa 37 wa Israel kutoka Uturuki kama 'ushindi
Ujumbe wa Erdogan 'Azerbaijan haiko peke yake' ulipelekea ushindi wa Karabakh: Aliyev
Ushindi wa Karabakh wa Azerbaijan kwa amani ya Caucasus: Rais Erdogan
Uturuki yatoa hati ya kukamatwa kwa Waziri Mkuu wa Israel Netanyahu, juu ya mashtaka ya mauaji
Erdogan: Uturuki kuharakisha miradi ya kiulinzi kuimarisha ‘maslahi’ na washirika wa Ulaya
Uturuki kuandaa mazungumzo ya Gaza wiki ijayo kufuatia wasiwasi juu ya usitishaji mapigano – Fidan
Mfumo wa ulimwengu wa sasa unazingatia nguvu zaidi ya haki: Mkurugenzi wa TRT
Israel imeigeuza Gaza kuwa vifusi, inawezaji kuwa haina hatia: Erdogan
Uturuki yakashifu unafiki wa nchi za Magharibi kuhusu Gaza, yatoa wito wa mfumo mpya wa dunia
Hamas haina nuyklia, Israel iko nayo: Erdogan aitaka Berlin ichukue hatua kali dhidi ya Tel Aviv
Erdogan ataka kuona mabadiliko katika uhusiano na EU na ushirikiano wa kikanda alipokutana na Mertz
Ujerumani yatoa wito wa kuunda “ushirikiano wa kimkakati” ili kukabiliana na changamoto za kimataifa
"Marekebisho ya Ulimwengu": Jukwaa la 9 la TRT World kuanza Istanbul likiangazia majadiliano na haki
Erdogan ametangaza washindi wa Tuzo Kuu za Utamaduni na Sanaa za Urais mwaka 2025
Uturuki yaadhimisha miaka 102 tangu kuanzishwa kwa Jamhuri
Uturuki yatoa wito wa kusitishwa mara moja kwa mapigano katika mji wa Al Fasher, Sudan
Uturuki na Jordan zasaini makubaliano ya kuimarisha uhusiano wa kiuchumi