| Swahili
UTURUKI
2 dk kusoma
Uturuki yatangaza kupatikana kwa kisanduku cheusi cha ndege iliyomuua Mkuu wa Jeshi wa Libya
Mchakato wa kuchunguza na kutathmini vifaa hivi umeanza, amesema Waziri wa Mambo ya Ndani, Ali Yerlikaya.
Uturuki yatangaza kupatikana kwa kisanduku cheusi cha ndege iliyomuua Mkuu wa Jeshi wa Libya
Waziri wa Mambo ya Ndani wa Uturuki, Ali Yerlikaya, atangaza kupatikana kwa kisanduku cheusi kufuati ajali ya ndege iliomuua mkuu wa jeshi wa Libya./ / AA
24 Desemba 2025

Waziri wa Mambo ya Ndani wa Uturuki, Ali Yerlikaya, ametangaza kupatikana kwa kisanduku cheusi (Black box) na kinasa sauti cha rubani mapema siku ya Jumatano kutoka kwenye mabaki ya ndege binafsi iliyoanguka karibu na Ankara, Uturuki, usiku wa Jumanne.

Mkuu wa Jeshi wa Libya na watu waliokuwa ndani ya ndege hiyo wamefariki dunia.

“Kutokana na kazi zilizofanywa katika eneo la tukio na maafisa kutoka Kituo cha Uchunguzi wa Usalama wa Usafiri wa Wizara ya Uchukuzi na Miundombinu, kinasa sauti cha ndege kilipatikana katika eneo la mabaki saa 8:45 usiku, na kisanduku cheusi kimepatikana saa 9:20 usiku,” alisema Waziri huyo.

Waziri huyo aliongeza kwamba mchakato wa kuchunguza na kutathmini vifaa hivi umeanza.

Jumla ya watu 408 wamekuwa wakifanya kazi katika eneo hilo wakitumia magari 103 na ndege 7.

Wajumbe 22 kutoka Libya – ikiwa ni pamoja na familia watano wa waliokufa, wawakilishi wa Wizara ya Ulinzi na maafisa kutoka Wizara ya Mambo ya Ndani – wamewasili Ankara, alisema Yerlikaya.

“Sisi pia tuna hamu sana kujua sababu ya ajali, lakini data hii itabaini sababu, na mamlaka itashiriki matokeo na nyinyi,” alisema.

Waziri huyo pia alitoa salamu za rambirambi kwa familia wa waliofariki dunia na kwa serikali na wananchi wa Libya, akieleza tukio hilo kama “ajali ya kusikitisha.”

Yerlikaya hapo awali amesema ya kwamba mabaki ya ndege ya binafsi ya aina ya Falcon 50, iliyotokea kutoka Uwanja wa Ndege wa Esenboga Ankara kuelekea Tripoli, yalipatikana vikosi vya usalama vya Uturuki takriban kilomita 2 kutoka kusini mwa kijiji cha Kesikkavak katika wilaya ya Haymana.

Serikali ya Umoja wa Kitaifa ya Libya ilitangaza siku tatu za maombolezo ya kitaifa kufuatia vifo hivyo.

Soma zaidi
Uturuki yafichua maelezo ya mpango wa uchimbaji visima pwani ya Somalia
Waliowasababishia mateso watu wa Gaza ‘watawajibishwa’: Erdogan
Shirika la Ndege la Uturuki kujenga kituo kikubwa zaidi cha mizigo kwa zaidi ya bilioni $2.3
Fidan na Kalin wa Uturuki wakutana na Umerov wa Ukraine jijini Ankara
Zaidi ya watu 500,000 waandamana kuiunga mkono Palestina mjini Istanbul katika siku ya Mwaka Mpya
Uturuki kuruhusu viza bila malipo kwa raia wa China
Uturuki kuendeleza juhudi za amani na diplomasia mwaka 2026: Fidan
Uturuki haitakubali uchokozi katika eneo la Mediterania ya Mashariki: Rais Erdogan
Uturuki yaanza ujenzi wa kituo cha anga ya juu nchini Somalia: Waziri
Somalia inapongeza mkataba wa kuchimba mafuta na Uturuki kabla ya shughuli za baharini za 2026
Uturuki yapinga hatua ya Israel kuhusu Somaliland, yaahidi kuimarisha ushirikiano na Somalia
Balozi wa Somalia nchini Uturuki anapongeza uungwaji mkono wa serikali ya Uturuki
Uturuki na Armenia zakubaliana kurahisisha utoaji wa viza katika jitihada za kuimarisha uhusiano
Rais wa Uturuki apongeza 'juhudi za ujenzi mpya' wakati wa utoaji wa nyumba za waathiriwa 455,000
Jamii ya Waturuki yafungua msikiti mpya nchini Uganda
Uturuki inazindua mpango wa kwanza wa kitaifa wa kujiandaa na maafa kwa watoto
Uturuki inafanya maombi mjini Ankara kwa ajili ya wajumbe wa Libya waliofariki
Uturuki inalaani Israel kwa kutambua Somaliland
Uwanja wa ndege wa Sabiha Gökçen umehudumia abiria milioni 44.2 katika kipindi cha miezi 11
Wachunguzi wapekua eneo la ajali ya ndege iliyomuua Mkuu wa Jeshi la Libya