| swahili
AFRIKA
1 dk kusoma
Mataifa ya G7 walaani mashambulizi ya RSF dhidi ya raia Sudan, watoa wito wa kusitishwa mapigano
Mawaziri wa mambo ya nje wa matafia ya G7 Jumatano wamelaani vikali mashambulizi wanayoyaita “ya kikabila” yanayotekelezwa na wapiganaji wa RSF dhidi ya raia na wafanyakazi wanaotoa misaada katika miji ya El-Fasher na Kordofan Kaskazini.
Mataifa ya G7 walaani mashambulizi ya RSF dhidi ya raia Sudan, watoa wito wa kusitishwa mapigano
Mzozo wa umwagaji damu kati ya jeshi na RSF, ambao ulianza Aprili 2023, umesababisha vifo vya watu wasiopungua 40,000. /
13 Novemba 2025

“Tunalaani vitendo vya ukatili wa kingono. Tunazitaka RSF na Jeshi la Sudan (SAF) kuheshimu haki za binadamu, kupunguza mapigano, kukubaliana juu ya usitishaji wa mapigano wa haraka na wa kudumu, na kuruhusu misaada ya kibinadamu kufika kwa haraka na bila vizuizi,” ilisema taarifa hiyo.

Mawaziri hao pia walionyesha uungwaji mkono wao kwa “jitihada za kidiplomasia zinazoendelea kurejesha amani na usalama,” na wakazitaka nchi nyingine kushiriki katika juhudi hizo.

Haya yanajiri baada ya Umoja wa Mataifa ukionya kuwa hali nchini Sudan inazidi kuwa mbaya kwa raia, huku mashirika ya misaada yakionyesha kuwa ufikiaji wa maeneo yaliyoathiriwa bado unazuiliwa na vita.

Mzozo wa umwagaji damu kati ya jeshi na RSF, ambao ulianza Aprili 2023, umeua watu wasiopungua 40,000 na wengine milioni 12 kuyahama makazi yao, kulingana na Shirika la Afya Ulimwenguni.

Mwezi uliopita, RSF iliteka mji mkuu wa jimbo la Darfur Kaskazini, El-Fasher, na kutuhumiwa kwa mauaji.

Kundi hilo linadhibiti majimbo yote matano ya Darfur kati ya majimbo 18 ya Sudan, wakati jeshi linashikilia majimbo 13 yaliyosalia, pamoja na Khartoum.

CHANZO:AA
Soma zaidi
Cape Verde, Mauritius na Ushelisheli wafanikiwa kuangamiza surua na  rubela
Rais wa Sudan Kusini Kiir amrejesha makamu wa rais katika mabadiliko ya baraza la mawaziri
Zaidi ya watu 100,000 wamekimbia makazi yao kutoka Al Fasher ya Sudan tangu kutwaliwa na RSF
Rais wa Tanzania amteua binti na mkwe wake katika Baraza la Mawaziri
Rais Samia amteua waziri mpya wa fedha, awaacha mawaziri wa mambo ya nje na madini madarakani
Tovuti za taasisi za serikali ya Kenya zashambuliwa
Mgodi waporomoka DRC na kuua watu wasiopungua 32
Wahamiaji 4 wafariki baada ya boti mbili zilizokuwa zimebeba makumi ya watu kuzama pwani ya Libya
Kikundi cha matabibu kinaripoti visa ya ubakaji wa wasichana wa Al Fasher baada ya RSF kuteka
Mlipuko wa virusi vya Marburg umethibitishwa kusini mwa Ethiopia
DR Congo, M23 wasaini makubaliano ya amani 'ya kihistoria' nchini Qatar
Baraza la Maaskofu Tanzania lataka uwajibikaji kwa waliohusika na mauaji ya waandamanaji
Baraza la usalama la UN laongezea mwaka mmoja ujumbe wa amani wa Abyei
Kiongozi wa zamani wa waasi wa DRC anayeshtakiwa Paris kwa uhalifu wa kivita aanza mgomo wa kula
UN yaagiza uchunguzi wa dharura ufanyike kuhusu ukiukaji wa sheria katika Al Fasher ya Sudan
Rais wa Tanzania atangaza uchunguzi kuhusu mauaji ya waandamanaji katika uchaguzi
Wakimbizi 57,000 wamewasili kaskazini mwa Sudan baada ya mashambulizi ya RSF huko Darfur, Kordofan
Afrika Kusini yaruhusu kuingia kwa wakimbizi zaidi ya 150 kutoka Gaza, Palestina
Afrika yakumbwa na mlipuko wa kipindupindu mbaya zaidi katika miaka 25
Wakenya zaidi ya 200 wajiunga na jeshi la Urusi