| Swahili
Jeshi la Sudan ladhibiti Ikulu ya Rais jijini Khartoum
Afrika
Jeshi la Sudan ladhibiti Ikulu ya Rais jijini Khartoum
Uhasama kati ya jeshi la Sudan linaloongozwa na Jenerali Abdel Fattah al-Burhan dhidi ya kikosi cha RSF umeanza mwezi Aprili 2023.
21 Machi 2025

Jeshi la Sudan latangaza kuchukua tena Ikulu ya Rais huko Khartoum, ikulu hiyo ni ngome ya mwisho iliokuwa ikidhibitiwa na kikosi cha RSF kinachoongozwa na  Mohammed Hamdan Dagalo.

Aidha, video na picha zimesambaa katika mitandao ya kijamii zikionyesha wanajeshi wa Sudan wakiwa ndani ya Ikulu kama ishara ya udhibiti huo.

Vita ndani ya jiji la Khartoum vimekua vikiendelea kwa kasi baada ya jeshi kuweza kuchukua udhibiti wa jimbo la Aljazeera na miji iliyokuwa karibu na Khartoum.

Uhasama kati ya jeshi la Sudan linaloongozwa na Jenerali Abdel Fattah al-Burhan dhidi ya kikosi cha RSF umeanza mwezi Aprili 2023, na kusababisha mgogoro mkubwa Sudan, huku watu wengi wakilazimshwa kuyahama makazi yao.

Tazama Video zaidi
Hatimaye mlipuko wa volkano ya Hayli Gubbi ya Ethiopia wapungua
Rais Samia atangazwa mshindi
Mwinyi ashinda uchaguzi Zanzibar
Kura zinaendelea kuhesabiwa Tanzania
Ulinzi mkali jijini Dar es Salaam kufuatia Uchaguzi Mkuu
Raia wa Tanzania waanza kupiga kura
Kampeni zakamilika Tanzania
'Coco Beach': Maisha yanasonga kawaida
Kasi ya biashara yapungua jijini Dar es Salaam Kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025
Tanzania: Wito wa amani watolewa kwa Uchaguzi Mkuu 2025